Jana mida ya Jioni pale mlimani City
nimeshuhudia wafanya kazi wa Duka Kubwa la Shoprite wakiwa wamegoma
wakizua watu wasiingie kwenye duka hilo kwa kile kilichodaiwa kuwa duka
hilo limeuzwa bila wao kupewa mafao yao …Habari zilizopo ni kuwa duka
hilo limenunuliwa na Super Market Ingine kubwa Nchini Kenya Ambayo
inakuja kupanua biashara zake hapa Dar …..
IMEELEZWA kuwa Tanzania ni miongoni
mwa wazalishaji wakubwa wa magadi soda yatakayoingizia taifa Shilingi
Bilioni 480 kwa mwaka. Hayo yamesemwa na Meneja Uhusiano na Mawsiliano
wa Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC), Abel Ngapemba akizungumza kwenye
mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Ngapemba alisema hatua hiyo inatokana
na kugunduliwa kwa kwa kiasi kikubwa cha madini hayo katika Bonde la
Engaruka Wilayani Monduli mkoani Arusha. Alizitaja faida za kugundulika
kwa madini ya magadi soda kuwa ni ajira zaidi ya 500 na fedha za kigeni
kutokana na mauzo ya madini hayo nje ya nchi.
Alisema kuwa viwanda vinavyotegemea
magadi soda kama malighafi ya uzalishaji hali itakayochochea kukua kwa
sekta ya viwanda hapa nchini. Ngapemba alibainisha kuwa madini ya magadi
soda yanatumika viwandani katika utengenezaji wa bidhaa kama vioo,
sabuni, dawa za meno, dawa za hosipitali, uoakaji mikate, kutengeneza
karatasi, nguo, na usafishaji wa maji.
Alifafanua kuwa utafiti uliofanywa na
wataalamu wazalendo kuanzia mwaka 2010 hadi 2013 na ulifanyika kwa awamu
tatu yakwanza ikiwa ni uchunguzi wa awali na kutafuta maeneo ya
kufanyia uchorongaji ili kubaini wingi na ubora wa magadi soda. Alisema
kuwa kazi iliyofanywa na kampuni ya OC, ambapo awamu iliyofuata ni
kuangalia njia ya uvunaji wa magadi soda hayo iliyofanywa na JSC
Service.
"Matokeo ya utafiti huo yameonyesha
kuwapo kwa magadi soda kiasi cha mita za ujazo bilioni 4.7 na
inakadiriwa kila mwaka wastani wa mita za ujazo milioni 1.9 zinaongezeka
katika eneo hilo," alisema Ngapemba na kuongeza: Alisema kuwa NDC
itahakikisha kuwa katika utekelezaji wa miradi hii mazingira
hayataathiriwa na tunu za taifa zitalindwa ambapo mtazamo wa shirika
hilo ni kuwapo kwa mradi wa uvunaji magadi, utalii, na ufugaji.
CHANZO:The Habari.com






Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizindua Bwawa la Maji la Mkata wilayani Handeni leo
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua baadhi ya madume bora ya
ng’ombe na kisha kuwakabidhi baadhi ya wafugaji katika kijiji cha
Msomela wilayni Handeni leo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza mmoja wa wafugaji
mwenye asili ya kimasai bwana Shayo Lahoda aliyegawiwa dume bora la
ng’ombe katika kijiji cha Msomela wilayani handeni leo
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na ngoma za utamaduni baada ya kuzindua Bwawa la Maji la Mkata wilayani Handeni leo
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua Bwawa la maji la Mkata
muda mfupi baada ya kulizindua huko Mkata wilayani Handeni Mkoa wa Tanga
leo asubuhi.Rais Kikwete yupo Mkoani Tanga kwa ziara ya kikazi kukagua
na kuzindua miradi ya maendeleo. Picha na Freddy Maro wa Ikulu


Baada
ya kutokea vurugu zilizosababishwa na baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalum
kupelekea Mwenyekiti wa Tume ya Marekebisho
ya Katiba Jaji Joseph Warioba (pichani juu, akiongozwa kutoka Bungeni
baada ya zoezi la kuwasilisha rasimu ya katiba
kuahirishwa) kutokuwasilisha rasimu ya pili ya Katiba kwa wajumbe hao,
Mwenyekiti wa Bunge Maalum Mhe. Samuel Sitta aliitisha kikao cha
maridhiano na baadhi ya wajumbe wanaowakilisha makundi mbalimbali
yaliyopo katika Bunge hilo ili kupata muafaka wa hoja zilizokuwa
zimejitokeza.





