Tuesday, February 18, 2014

SH14BILIONI KUSAMBAZA UMEME

seif_rashid_b6653.jpg
Rufiji. Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid amesema mwishoni mwa mwezi huu Serikali itatumia Sh4 bilioni kwa ajili ya kusambaza umeme katika vijiji 14 vilivyopo kwenye Kata ya Ikwiriri na Mloka mkoani Pwani.
Akizungumza jana wakati alipokutana na wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanzania(Tanesco) wa Wilaya ya Rufiji walipokuwa kwenye sherehe ya kuuaga mwaka 2013 na kuukaribish mwaka huu, Dk Rashid alisema mradi huo utatekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini(REA) ambapo watasambaza katika vijiji hivyo mwishoni mwa mwezi huu .
Alisema katika utekelezaji wa mradi huo, huduma za kijamii zitapewa kipaumbele katika kuunganishiwa nishati hiyo ikiwamo shule, zahanati, Visima vya maji, misikiti na makanisa na kwamba mradi huo wa umeme utainua kiwango cha ubora wa maisha ya wananchi. chanzo MWANANCHI

No comments:

Post a Comment