Monday, March 24, 2014

SHOPRITE IMEUZWA WAFANYA KAZI WAGOMA NA KUANDAMANA MLIMANI CITY

Jana mida ya Jioni pale mlimani City nimeshuhudia wafanya kazi wa Duka Kubwa la Shoprite wakiwa wamegoma wakizua watu wasiingie kwenye duka hilo kwa kile kilichodaiwa kuwa duka hilo limeuzwa bila wao kupewa mafao yao …Habari zilizopo ni kuwa duka hilo limenunuliwa na Super Market Ingine kubwa Nchini Kenya Ambayo inakuja kupanua biashara zake hapa Dar …..

UTABIRI WA TB JOSHUA WATIMIA-NI KWELI AIR MALAYSIA ILIANGUKA INDIAN OCEAN NA HAKUNA ALIYE PONA

Baada ya ndege ya Air Malaysia kupotea Mtabiri TB Joshua Alisema Kuwa Ndege hiyo itakuwa imeanguka Kwenye Bahari ya Hindi na Hakuna Aliyepona ,,,Utabiri huo kwa wengi ulichukuliwa kama mzaha lakini leo imedhihirika tena kwa mara nyingine kuwa utabiri wake ni wa Kweli , kwani imethibitika kuwa ndege hiyo ilianguka kwenye bahari hiyo na hakuna aliye pona...

WEWE UNAYETESEKA NA KUUMWA MENO,KUNUKA MDOMO,NA UNENE AU MANYAMA UZEMBE SOMA HAPAA

Je?unasumbuliwa na matatizo ya kinywa,harufu mbaya na meno yanayouma??Yaliyotoboka na yanatakiwa kung'olewa??Usiumize kichwa wala akili yako,tiba ipo bila kung’oa..Na je unapenda kupunguza uzito Hadi kilo 9 kwa siku nane tu?Siyo miujiza wala uchawi na vyakula na maelekezo tu..piga namba 0784-778788 upate tiba na ushauri namna ya kufanya uondokane na tatizo hilo.

ZITAMBUE NJIA 5 RAHISI ZA KUISHI MAISHA YENYE FURAHA NDANI YA NDOA.

http://lovestruckguru.com/wp-content/uploads/2011/08/istock_relationships.jpg
1. Usiwe na hisia zinazopita kiasi= Bali kuwa na Imani
2. Kamwe usikate tamaa= Endelea kujaribu
3. Usifanye mambo kuwa magumu= Chukulia kawaida tu


4. Usichukulie vitu kwa umakini kupita kiasi= Yacheke matatizo.
5. Siku zote usikue= Ishi kama mtoto/kijana.



NAMNA YA KUJENGA NDOA YENYE FURAHA NA MAFANIKIO.


:Mara zote vijana na wale wote wanaoowa ama kuolewa huwa na shauku kuu ya kutaraji na kuwa na matumaini kuwa ndoa yao itawaletea maisha yenye furaha.

Miezi mitatu mpaka sita baadae wanandoa hawa hubaini kuwa ndoa si jambo jepesi,kumbe ndoa ni jambo linalohitaji subira ya hali ya juu.Vifuatavyo ni vidokezo muhimu vitakavyosaidia mume na mke kujenga mahusiano mazuri na yenye furaha.

INGIA KATIKA MAHUSIANO YA NDOA UKIWA NA NIA THABITI,NA KILA MARA IFANYE MPYA NIA YAKO;

Mnapaswa kuyaingia maisha ya ndoa mkiwa na nia safi ya kutafuta radhi za Allah (SW) pamoja na rehma na baraka zake kwa kukusudia kwamba ndoa ni kitu cha kudumu,kufanya hivyo ndoa yenu hugeuka kuwa ibada kitu ambacho kitakuwa kikiwapatia thawabu,nia thabiti ni jambo la msingi litakalowahakikishia amani,umadhubuti wa penzi pamoja na furaha katika muda wote wa maisha yenu ya ndoa.


Na kwakuwa tendo hili ni ibada kila mara ifanyeni mpya nia yenu ili kuhakikisha ya kuwa hamtoki nje ya mstari na kukosa faida zitokanazo na uhusiano aupendao Allah (SW)

KUMBUKA PIA MKE WAKO NI NDUGUYO KATIKA UISLAMU:
Mara nyingi waislamu wamekuwa wakiwajali zaidi watu wa nje ya familia yao, kwa wema na uaminifu lakini huwa na tabia tofauti kabisa anapokuwa na mwenzi wake hili si jambo zuri kwani hupelekea kuchokana haraka,Waislamu wanapaswa kuelewa kuwa mpenzi wako katika uislamu ni nduguyo,unapaswa kumtimizia kwa kukamiliha wajibu wako.Jitahidi kuzielewa ipasavyo haki za udugu wa kiislamu na kuzifata kimatendo.

HIMIZA YALIO BORA KWA MPENZI WAKO:
Kwa kuwa hakuna mwanadamu aliyetunukiwa kila aina ya ubora autakao,basi hamasa iwekwe kwa ule ubora alio nao Asali wako wa moyo,Jitahidi kumtia moyo,kumsifia na kuonesha kuridhishwa na ubora alio nao kila mara,kufanya hivi kutaimarisha ubora wake na kumpa fursa ya kuendeleza vipaji vyengine vya ubora alio nao.Jitahidi kutoyatilia maanani mapungufu madogo madogo aliyo nayo mpenzi wako,yasije kumnyima furaha.


''KAMA ALIVYOSEMA MTUME (SAW) KUWA:''MWANAMME MWENYE KUAMINI ASIMDHURU MWANAMKE MWENYE KUAMINI,KWANI ANAWEZA KUCHUKIZWA NA TABIA MOJA LAKINI AKAMPENDA NA KUMRIDHIA KWA TABIA NYENGINE.''(Muslim)


KUWA RAFIKI WA KARIBU WA MPENZI WAKO:
Tafakari vipi rafiki wa karibu anapaswa kuwa(best friend) kisha uwe hivyo kwa mwenzi wako,hii inajumuisha kushirikiana katika anavyovipenda,kuujua uzoefu wake,ndoto zake za kimaisha,matatizo yake na hata kukata tamaa kwake.


Na hili linawezekana tu pale unapojua mahitaji ya mpenzi wako (anapenda nini hapendi nini) kisha umsaidie kadiri itakavyowezekana.kwani rafiki wa karibu ni mtu unaepaswa kumtunzia siri,kumwamini,kumtegemea katika maisha,hivi ndivyo mpenzi wako anavyohitaji katika maisha yenu ya kila siku.

USIWEKE MATARAJIO YASIO WEZEKANA KWA MWANDANI WAKO:
Mara nyingi kabla ya ndoa watu wengi huwa na mawazo ya kinjozi,kuhusu mke au mume mtarajiwa wengi hutegemea kumwona awe amekamilika kila nyanja,katika uhalisia ni vigumu kumpata mtu aliye kamilika kwa kila jambo.Vinginevyo mawazo hayo husababisha kero na matatizo yasio na muhimu katika ndoa yako.


Yafaa tuzingatie Allah( sw) amemjaalia mwanadamu kuwa ni mwenye mapungufu mengi hivyo tutegemee kasoro nyingi,kwa kuzingatia hili la mapungufu ya kibinadamu na kujitahidi kwako kurekebisha mapungufu hayo ya mwenzio,basi uatashangazwa na kuona ndoa yenu itakavyokuwa na maridhiano.

TUMIENI MUDA WA THAMANI PAMOJA:
Mnapaswa kutafuta muda wa ziada katika ratiba zenu ngumu za kimaisha ,kuimarisha penzi lenu kwa kuwa pamoja,na muda wa thamani unaokusudiwa hapa ni kama vile kufanya safari fupifupi pamoja ,au hata kufanya shughuli itakayoruhusu uwili wenu nje ya maisha ya nyumba yenu na mengine mengi mfano wa hayo.


ONESHA HISIA ZAKO MARA ZOTE:
Njia ya mawasiliano yenu yapaswa kuwa wazi na tayari kupokea hisia za mwenzi wako kila zinapoibuka,hii nitiba mujarab ya nafsi,Lakini kuna hatari kubwa kunyamazia hisia za mwenzi wako hasa za kimapenzi.Jitahidini kukidhiana haja.


KIRI MAKOSA NA JENGA TABIA YA KUOMBA MSAMAHA:
Kama tufanyavyo katika kumuomba Allah (sw) msamaha kila mara tukoseapo,hivyo ndivyo tunapaswa kufanya kwa wapenzi wetu,kwani mtu mara na mwenye nguvu ni yule ambae yuko tayari kukiri pale anapokosea,na kisha kuomba msamaha.


Baada ya hapo ongeza juhudi kuboresha yale yote yanayoongeza mapenzi,mwanandoa asiye tayari kufanya hivi ategemee maendeleo duni yakimahaba katika ndoa yao.


USIPENDE KUIBUA MAKOSA YA WAKATI ULIO PITA:
Uislamu unakataza mtu kujikita na kusimamia mambo yalio kwisha pita.Mtu anapaswa ayakumbuke makosa yaliyopita ili yasije yakarejewa tena,lakini hili lisiwe linafanywa kupita kiasi,bila shaka sisi kama binadamu hatuna haki yakuwahukumu bianadamu wenzetu.twaweza kuwashauri tu tena kwa kuzingatia maadili.


BAADHI YA WAKATI MSTAAJABISHE MKE WAKO:
Kuna namna nyingi za kumstaajabisha mpenzi wako,kama kumlete zawadi ndogondogo au hata katika muda ambao hakuutegemea,au kumuandalia mlo maalum au kumvalia mavazi ya kupendeza au kujipendezesha,kwa naman nyengine yoyote aipendayo mahabubu wako,hii ni ka wanawake na wanaume. 


Lengo kuu ni kuyatia ladha mapenzi na uhusiano wenu wa kindoa kwa kuepusha kwa kupesha ratiba zenye kuchosha.

KUWA NI MWENYE MZAHA NA UTANI BAADHI YA NYAKATI:
Uchangamfu,ucheshi,na utani usiopindukia mipaka ya uislamu kwani ni miongoni mwa mambo yanayoongeza ladha ya mapenzi katika ndoa,utani huzuia mabishano na hufungua nuru ya mapenzi katika familia,Kwa kuwa maisha ni mkondo wenye changamoto nyingi na mitihani,kuyaendea vyema maisha hayo humuia rahisi yule mwenye moyo mkunjufu na uliojaa maskhara ya kimapenzi.


Hata kama upatikanaji riziki yenu ni mdogo basi utamuona mwandani wako hachoki kuwa nawe popote utapokwenda.

100 wakamatwa mjini Mombasa, Kenya

140212145434_mombasa_vijana_304x171_bbc_nocredit_92a51.jpg
Watu 100 wamekamatwa mjini Mombasa Pwani ya Kenya kufuatia mashambulizi yaliyofanywa ndani ya kanisa moja mjini humo siku ya Jumapili. Watu waliokuwa wamejihami kwa bunduki na kufunika nyuso zao waliwapiga risasi waumini wa kanisa moja mtaani Likoni na kuwaua watu wanne Watu  walifariki papo hapo wengine wakifariki hospitalini wakati wakipokea matibabu. Wengine 17 walijeruhiwa vibaya.
Polisi wanasema kuwa watu watatu waliokuwa wamejihami walivamia kanisa la Joy Jesus na kuanza kuwafyatulia waumini risasi kiholelea. Kadhalika polisi walisema kuwa washukiwa wakuu wa shambulizi hilo wametoweka 
Hakuna mtu yeyote aliyekiri kufanya mashambulizi hayo , ila Kenya imekuwa ikishuhudia ongezeko la mashambulizi tangu kuanza kujihusisha na vita nchini Somalia mwaka 2011. Jeshi la Kenya linasaidiana na wanajeshi wa Muungano wa Afrika kupambana na kundi la wanamgambo la Al Shabaab.
Hali ya usalama imedhibitiwa mjini humo kufuatia shambulizi hilo ambalo limekuja siku chache tu baada ya polisi kunasa washukiwa watatu wa ugaidi wakiwa na mabomu mawili makubwa tayari kufanya shambulizi kubwa. Pia walinasa vilipuzi vingine ndani ya gari lililokuwa limeegeshwa karibu na kituo cha polisi. Mji wa Mombasa wenye sifa ya utalii, umekuwa ukikumbwa na suitofahamu ya kiusalama kutokana na vijana wengi kujiunga na itikadi kali za dini hiyo.

Sunday, March 23, 2014

Ebola ni kiini cha ugonjwa hatari nchini Guinea


Wanasayansi nchini Ufaransa wamebaini kwamba virusi vya Ugonjwa wa Ebola ndio chanzo cha ugonjwa wa homa ya haemorajic nchini Guinea ambayo inaaminika kuwauwa karibia watu sitini.
Ugonjwa huo ambao unaweza kuambukizwa kwa haraka ulianza nchini humo yapata majuma sita yaliopita.
Dalili za ugonjwa huo ni kutoka damu,kuharisha pamoja na kutapika.
Afisa mmoja wa wizara ya afya nchini Guinea amesema kuwa takriban visa vinane vya ugonjwa huo vimeripotiwa hususan kusini mwa taifa hilo.
Amsema kuwa serikali ya taifa hilo inatumia kila njia kukabiliana na ugonjwa huo lakini inaendelea kushindwa.
Kufikia sasa hakuna tiba ya ugonjwa wa Ebola ambao husambazwa kupitia kugusana na walioambukizwa

MABANDA YANAYOONESHA VIDEO ZA NGONO YAFUTIWA LESENI

Serikali mkoani Pwani  imefuta vibali vya uendeshaji wa mabanda ya kuonyesha  video wilayani Kibaha pamoja na kuanzisha  uchunguzi wa wanafunzi wa shule  msingi wanaojihusisha na vitendo vya ulawiti.
 
Hatua hiyo inachukuliwa  baada ya wanafunzi wa kiume wa shule za msingi wilayani humo kudaiwa kufanya vitendo hivyo vyenye athari kiafya na kitaaluma.
 
Katika hatua nyingine, polisi wilayani humo inawashikilia watu wawili  waliokutwa wakiendesha biashara ya kuonyesha video chafu kwenye mabanda kinyume na sheria.
Toleo la Nipashe la Jumapili iliyopita liliripoti  taarifa za wanafunzi  katika shule tatu zilizopo Mlandizi, wilayani humo wanaojihusisha na  vitendo vya kujaamiana kinyume cha maumbile wenyewe kwa wenyewe, pamoja na watu wengine kutoka nje ya shule hizo wakiwadhalilisha kingono.
 
Taarifa za uhakika zilisema tayari timu maalum imeundwa na uongozi wa mkoa huo kwa ajili ya kuchunguza suala hilo na wajumbe watatembelea  shule zilizotajwa katika  mahojiano na wanafunzi pamoja na walimu.
 
Akizungumza na NIPASHE, Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kibaha, Amedeus Marenge, alisema pamoja na kushikiliwa watuhumiwa hao wawili,  wamefungua jalada  la uchunguzi katika shule mbalimbali wilayani humo kubaini washukiwa.
 
Alisema wanaoshikiliwa siyo kwamba wanahusika moja kwa moja na tuhuma hizo, bali mabanda wanayoyamiliki yanatumiwa kudhalilisha watoto na kuonyesha picha zisizo na maadili.
 
"Kazi ya kuchunguza suala kama hili ni ngumu kwa sababu mambo yote yanafanyika sirini na hakuna  aliyejitokeza kusema ukweli. Uchunguzi wetu unaendelea ….," Alisema Marenge.
 
Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya  aliwataka wananchi hasa wazazi kushirikiana na polisi kwa kutoa taarifa wanapoona mambo yanayowapa mashaka kuhusu mienendo ya watoto wao.
 
HALMASHAURI YAFUTA VIBALI
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kibaha, Tatu Selemani, alisema kuanzia sasa shughuli ya uonyeshaji video kwenye mabanda umepigwa marufuku.
 
Alisema amemuagiza Afisa Utamaduni kufuta vibali pamoja na kuwafuatilia wanaoonyesha picha hizo.
 
"Nimeagiza vibali vyote vifutwe na marufuku kwa kuendesha shughuli hiyo hata kama wana malengo ya kuonyesha soka,"alisema.
 
Uchunguzi wa gazeti hili uliofanywa maeneo hayo ulibaini mabanda mengi ya aina hiyo yamefungwa na kufuli.
 
WANANCHI WAPONGEZA 
Baadhi ya wazazi waliipongeza  serikali kuingilia kati na kuwanusuru wanafunzi ambao walianza kupotoka na kuongeza kuwa kusitishwa uonyeshaji wa picha za video kumewezesha watoto  kuanza kwenda shuleni.
 
"Viongozi wa serikali walikuja hapa Jumatatu na kufunga vibanda hivi jirani na shule za msingi Mtongani na Azimio, tumeanza kuona matokeo mazuri kwani watoto wanakwenda shule na kuhudhuria vipindi ," alisema Hamisi Kondo mkazi wa Mtongani.
Mzazi  mwingine Christopher Steven, aliwapongeza  wanafunzi na walimu walioibua suala hilo kwa kuowaokoa watoto wengi ambao wangeingia katika mazingira hayo hatarishi.
 
"Unajua sisi wazazi tumekuwa na tabia ya kutosikiliza yanayosemwa na walimu, badala yake tunasubiri hadi mambo yawe makubwa ndipo tunashtuka, naamini wanafunzi na walimu wametupa mwanga na nia yao ilikuwa kuokoa watoto wetu, tunashukuru," alisema Steven.
 
Uchunguzi huo ulioibua matukio hayo ulifanywa katika shule za msingi za Mtongani, Azimio na Jamhuri zilizoko  mji mdogo wa Mlandizi na yaliyohusisha wanafunzi wa  darasa la tatu na la nne ambao mara nyingi wanalazimishwa kulawitiwa na wenzao wa madarasa ya juu.
 
Aidha ilidaiwa wanafunzi wengine wanafanyiwa vitendo hivyo na watu wazima wakiwa majumbani kwao na kwenye mabanda yanayoonyesha picha za video nyakati za usiku.
 
Ilielezwa kwamba ndani ya mabanda hayo watoto waliingiliwa na watu wazima  baada ya kuangalia picha za ngono.
 
CHANZO: NIPASHE

MWENDESHA BODABODA AMGONGA MTU NA KUMVUNJA MGUU,ATIMUA MBIO NA KUTELEKEZA PIKIPIKI

Ajali mbaya ya pikipiki ambapo mwendesha Bodaboda amemgonga mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Heri Idd mkazi wa kata ya Ng'ambo manispaa ya Tabora,  Idd aligongwa na Bodaboda hiyo wakati akiwa barabarani akiendesha usafiri wake wa baiskeli na mara baada ya kugongwa na kuvunjika mguu,Mwendesha Bodaboda ambaye hakufahamika mara moja aliamua kukimbia na kuicha pikipiki yake imezunguukwa na umati wa watu huku majeruhi akipatiwa msaada wa kupelekwa hospitali ya mkoa wa Tabora Kitete kwa ajili ya matibabu.  

Heri Idd akiwa amelazwa wadi ya majeruhi hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete.(Picha zote na Mpiga picha wetu)

ZIARA YA RAIS KIKWETE MKOANI TANGA, AZINDUA BWAWA LA MAJI MKATA HANDENI


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgAnT5ZogvHDE4agrY0hBEC7jPsrSKR8xRIgPlr9jDd_4-JuT-l__KKfT8Zvhfmu08uUe9QLwVVAclkCcWb2Ufcvd-eCT8-klIbetp7pGiK52AU7F1KqxtuE3LtDTJPgX5raYYnANCDq1i2/s1600/unnamed+(78).jpg Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizindua Bwawa la Maji la Mkata wilayani Handeni leohttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjcjWbJ-G2wLEEKH1vytfvS-iwprPp6QFChKolwB3GOnFuI5ySsBd6yzzdzRWF0JhCIzPf0UbpqfjRBkiRKsXxyouY6gjbvEN0obns-yixrDk7A2H5G0Bi2sS6AmRyZ4p8VMUmtDJwPbBuK/s1600/unnamed+(86).jpgRais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua baadhi ya madume bora ya ng’ombe na kisha kuwakabidhi baadhi ya wafugaji katika kijiji cha Msomela wilayni Handeni leo.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiIhfT3CzMcrHSdACtFVEj-ZeBHM3aV7ZTeERLqCVS61Jm8lCI1F8tw7wKfag4RiwpJR5_WnEIvl_IN-F1TizmUfNMsoIxN4PyqbMmrFdNC-ZHeEwBLL16kIAK_4XOOZ2otXjWtmmHPIhno/s1600/unnamed+(87).jpgRais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza mmoja wa wafugaji mwenye asili ya kimasai bwana Shayo Lahoda aliyegawiwa dume bora la ng’ombe katika kijiji cha Msomela wilayani handeni leo
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgK9UO2qJ3TIEIahmmavslJl0J5rgKKtaG33vjUZbJH9zQ5f0GOlAvxuYhoAeJuw4XkexLuYHgt250lCfhwmgqZY79iy27YwVbQvSI8t8EMR28oa1TqqPolcTljH-RTd3cnEiDTOAuc_DL0/s1600/unnamed+(79).jpgRais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na ngoma za utamaduni baada ya kuzindua Bwawa la Maji la Mkata wilayani Handeni leohttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjE2iLyZaG0ynjcR6eTOeMtcADS1jOd_P_hgnBrFJyLJhjvZDwKPEgpSe5i7_tRo9DB7Y8c6SH4m1L5s_Z2I1qYb_-ycpm167Am6vS_1A-eYlNV_Fw-mkVXTR0jXKv-LO02nQpMA8eiJ8v5/s1600/unnamed+(80).jpgRais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua Bwawa la maji la Mkata muda mfupi baada ya kulizindua huko Mkata wilayani Handeni Mkoa wa Tanga leo asubuhi.Rais Kikwete yupo Mkoani Tanga kwa ziara ya kikazi kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo. Picha na Freddy Maro wa Ikulu

MESSI WA SIMBA AVUNJA MLANGO UWANJA WA TAIFA


 
Na Baby Akwitende, Dar es Salaam
KIUNGO mshambuliaji wa Simba SC, Ramadhani Yahya Singano ‘Messi’ anadaiwa kuvunja kioo cha mlango wa chumba cha kubadilishia nguo cha timu yake leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam baada ya mechi dhidi ya Coastal Union ya Tanga, Wakundu wa Msimbazi wakifungwa 1-0.

Pamoja na ushahidi uliotolewa na wafanyakazi wa Uwanja wa Taifa kwa askari Polisi kwamba, Messi ndiye aliyevunja kioo, hicho lakini wachezaji wenzake na viongozi wa Simba SC walimtetea.

Polisi walishindwa kuchukua hatua yoyote kuhofia kusababisha vurugu na mchezaji huyo aliondoka uwanjani hapo kuelekea kwenye basi la timu yake akisindikizwa na baunsa. 

Tukio hilo limechukuliwa kama hasira za kipigo cha bao 1-0 nyumbani mbele ya Coastal Union katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Tuesday, March 18, 2014

Madini ya Magadi Soda Kuiingizia Tanzania Bilioni 480

mmmmm_8f261.jpg
Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Abel Ngapemba akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO. Katikati ni mkuu wa kitengo cha viwanda vya Kemikali Muhandisi Abdallah Mandwanga, na Mwisho ni ofisa Habari wa Idara
mmmm3_72996.jpg
Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Abel Ngapemba akifafanua kwa waandishi umuhimu wa mradi wa uchimbaji magadi soda katika mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya habari MAELEZO. Kushoto ni Mhandisi wa mradi Godfrey Mahundi na Kulia ni mkuu wa kitengo cha viwanda vya Kemikali Muhandisi Abdallah Mandwanga. Picha na Georgina Misama – Maelezo.
IMEELEZWA kuwa Tanzania ni miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa magadi soda yatakayoingizia taifa Shilingi Bilioni 480 kwa mwaka. Hayo yamesemwa na Meneja Uhusiano na Mawsiliano wa Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC), Abel Ngapemba akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Ngapemba alisema hatua hiyo inatokana na kugunduliwa kwa kwa kiasi kikubwa cha madini hayo katika Bonde la Engaruka Wilayani Monduli mkoani Arusha. Alizitaja faida za kugundulika kwa madini ya magadi soda kuwa ni ajira zaidi ya 500 na fedha za kigeni kutokana na mauzo ya madini hayo nje ya nchi.
Alisema kuwa viwanda vinavyotegemea magadi soda kama malighafi ya uzalishaji hali itakayochochea kukua kwa sekta ya viwanda hapa nchini. Ngapemba alibainisha kuwa madini ya magadi soda yanatumika viwandani katika utengenezaji wa bidhaa kama vioo, sabuni, dawa za meno, dawa za hosipitali, uoakaji mikate, kutengeneza karatasi, nguo, na usafishaji wa maji.
Alifafanua kuwa utafiti uliofanywa na wataalamu wazalendo kuanzia mwaka 2010 hadi 2013 na ulifanyika kwa awamu tatu yakwanza ikiwa ni uchunguzi wa awali na kutafuta maeneo ya kufanyia uchorongaji ili kubaini wingi na ubora wa magadi soda. Alisema kuwa kazi iliyofanywa na kampuni ya OC, ambapo awamu iliyofuata ni kuangalia njia ya uvunaji wa magadi soda hayo iliyofanywa na JSC Service.
"Matokeo ya utafiti huo yameonyesha kuwapo kwa magadi soda kiasi cha mita za ujazo bilioni 4.7 na inakadiriwa kila mwaka wastani wa mita za ujazo milioni 1.9 zinaongezeka katika eneo hilo," alisema Ngapemba na kuongeza: Alisema kuwa NDC itahakikisha kuwa katika utekelezaji wa miradi hii mazingira hayataathiriwa na tunu za taifa zitalindwa ambapo mtazamo wa shirika hilo ni kuwapo kwa mradi wa uvunaji magadi, utalii, na ufugaji.
CHANZO:The Habari.com

JE?UNA MATATIZO LA KIAFYA KATIKA UZAZI??NGUVU ZA KIUME/KIKE JE?..SOMA HAPA UPONEEE...


Kilio cha kina Baba na Kinama  kusumbuliwa na upungufu mkubwa wa nguvu za kiume au kukosa hamu ya tendo la ndoa...hadi unahisi umeolewa au kuoa kwa bahati mbaya?kama ndiyo piga namba hii
 0784 -778788  upate package yako itakayokusaidia kuurudisha mwili wako katika hali yake ya kawaida bila madhara kwani virutubisho hivi siyo kemikali na kukusaidia kumridhisha mwenzi wako..

“Sina njaa….Sigombei tena”..Aden Rage

Wakati wanachama wa Simba wakipitisha mapendekezo ya marekebisho ya katiba yao, Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage ametangaza kutogombea tena nafasi hiyo jana asubuhi kwenye ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay.
Akizungumza kwenye mkutano huo wa marekebisho ya Katiba ya Simba, Rage alisema: “Simba oyee…Wanasimba msifanye makosa Mei 4 hakikisheni mnachagua kiongozi ambaye atakaa madarakani miaka minne, msifanye makosa baada ya mwaka mmoja mkataka aondoke, Katiba ya Simba inakataza mapinduzi.
“Mimi sitagombea, mimi siyo maskini, sina njaa, hata mkizomea nasemaje mimi sina njaa, na wanachama wengi mliopo hapa ni mambumbumbu.”
Kauli hiyo iliamsha hasira kwa baadhi ya wanachama ambao walitaka kumvamia na kumtwanga makonde, lakini Polisi waliingilia kati na kusababisha wanachama kupambana na wale wanaomuunga mkono Rage, tafrani hiyo ilidumu kwa zaidi ya nusu saa hadi pale Rage alipoomba radhi kwa kutangaza kuifuta kauli yake hali ikatulia na mkutano ukaanza.
RAGE
Ismail Aden Rage
Hata hivyo mkutano huo ulifanyika huku akidi ya wanachama ikiwa haijatimia kwani ili akidi itimie ilitakiwa kuwe na wanachama 250 na kuendelea, lakini wanachama waliofika jana ni 166 ambao hawafikii hata nusu ya akidi ya wanachama ambayo inatambulika kwa mujibu wa Katiba ya Simba.
Katika mkutano huo wanachama walipinga kuburuzwa kwa kuwepo kipengele cha ibara ya 11 (a) ambacho kinakataza mwanachama kuzungumza na vyombo vya habari isipokuwa vikao halali, na mwanachama atakayefanya hivyo tawi limuwajibishe ndani ya siku 14 tangu kutokea kwa kitendo hicho, wanachama hao waligoma na kutaka kifungu hicho kiondolewe kwani kinawaminya uhuru na haki ya kuzungumza.
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Geofrey Nyange naye alijikuta akizodolewa na Rage pale aliponyoosha kidole na kusema: “Taarifa mwenyekiti…taarifa, huku akisimama na kujibiwa na Rage ‘Siyo lazima usimame, kaa chini, nimesema siyo lazima, mwingine’ alisema Rage na kuteua mwanachama mwingine kuchangia hoja yake kabla ya kumpa nafasi Kaburu.
Akichangia kuhusu kipengele hicho Kaburu alisema: “Hakuna eneo ambalo TFF ilisema kuhusu kifungu hiki, haya ni mawazo yetu ni kweli baadhi ya wanachama wanatukana viongozi ndio maana kikawekwa ili kuminya wanachama wakorofi, kwa vile tupo hapa kwa ajili ya kuunda Kamati ya Maadili wakorofi wote watapelekwa kamati ya maadili ndio watawajibishwa huko siyo kuingiza kwenye katiba,” alisema Kaburu na kushangiliwa na wanachama wengi.
Kipengele kingine ambacho kinasubiri huruma ya TFF ambacho Simba wamekipitisha kwa kishindo ni kile cha ibara ya 26 kinachozungumzia sifa za wagombea, fasili ya tano ya katiba ya Simba ya zamani inasomeka: ‘Asiwe aliyewahi kutiwa hatiani kwa kosa la jinai kwa kuhukumiwa kifungo’.
Wanachama hao wametaka kifungo hicho kisomeke ‘Asiwe ametiwa hatiani kwa kifungo cha zaidi ya miezi sita bila mbadala wa adhabu na endapo ametiwa hatiani kwa kifungo cha zaidi ya miezi sita, awe amemaliza muda wa miaka mitano tangu kuisha kwa kifungo husika bila kutiwa hatiani kwa kosa lingine lolote la jinai.
Kipengele hicho (b) kimeongezwa maneno yanayosomeka: ‘Mgombea ni lazima awe ametimiza angalau mwaka mmoja wa uanachama na si miaka mitano kama ilivyo sasa.’

Mahakama Yatupilia mbali Ombi la Sheikh PONDA, Arudishwa Segerea…!!

Ombi la marejeo lililowasilishwa na Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda limetupiliwa mbali na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ilipotoa uamuzi wa pingamizi la awali lililowasilishwa na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), akidai kuwa ombi hilo halikuwa na msingi kisheria.
Kesi hiyo iliyosikilizwa kwa saa 1 na dakika 40 ilitolewa uamuzi na Jaji Augustine Mwarija.

Baada ya uamuzi huo, Sheikh Ponda alirudishwa jela huko Segerea jijini Dar akiwa chini ya ulinzi mkali wa Jeshi la Polisi.

sheikh ponda

HOT NEWS: TAARIFA MUHIMU KUHUSU KUENDELEA KWA KIKAO CHA BUNGE MAALUM LA KATIBA LEO TAREHE 18 MACHI, 2014

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgmYOiPgF1T3sMdwF20AVY0qnNohF_OErC0sICzmm3yXlHCa0G10oPB1PZyZJh2HUHSENRKE4CNTpRf0XKWCakkiMwwlKXu0TpEiohuQqZqUpAgir8YmVw_5D6JA76kUMBB4hBtyfcosSqG/s1600/unnamedj.jpgBaada ya kutokea vurugu zilizosababishwa na baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalum kupelekea Mwenyekiti wa Tume ya Marekebisho ya Katiba Jaji Joseph Warioba  (pichani juu, akiongozwa kutoka Bungeni baada ya zoezi la kuwasilisha rasimu ya katiba kuahirishwa) kutokuwasilisha rasimu ya pili ya Katiba kwa wajumbe hao, Mwenyekiti wa Bunge Maalum Mhe. Samuel Sitta aliitisha kikao cha maridhiano na baadhi ya wajumbe wanaowakilisha makundi mbalimbali yaliyopo katika Bunge hilo ili kupata muafaka wa hoja zilizokuwa zimejitokeza.

Baada ya kikao hicho kilichodumu kwa takribani masaa manne na kumalizika saa nne za usiku, Mhe. Samuel Sitta amewaeleza waandishi wa Habari matokeo ya kikao hicho, ambapo wajumbe wa kamati hiyo wameafikiana yafuatayo:

Kikao cha Bunge Maalum kitaendelea leo tarehe 18 Machi, 2014 Saa tatu asubuhi kwa kuanza na shughuli za kuapisha baadhi ya wajumbe ambao hawakuapa awali kwa muda wa dakika 30 Kuhusu muda wa kuwasilisha Rasimu ya Katiba, Wajumbe wameafikiana Mwenyekiti wa Tume ya Marekebisho ya Katiba Jaji Joseph Warioba kuwasilisha Rasimu ya pili ya Katiba kwa wajumbe hao kwa muda wa saa nne badala ya saa mbili alizokuwa ametengewa awali, ambapo uwasilishwaji wa rasimu huo utaanza rasmi saa tatu na nusu asubuhi baada ya shughuli ya viapo kumalizika.
 
Saa kumi kamili jioni kutakuwa na semina ya kanuni itakayofanyika katika Ukumbi wa Bunge ambapo Mwenyekiti wa iliyokuwa kamati ya kanuni Mhe. Prof. Costa Mahalu na wenzeke watawawezesha wajumbe kupitia vifungu vya kanuni hizo za Bunge Maalum, ambapo semina hiyo itaendelea hadi jumatano tarehe 19 machi, 2014 Siku ya Alhamisi tarehe 20 Machi, kutakuwa na semina itakayoendeshwa na maafisa wawili kutoka kenya ambao watatoa uzoefu wao katika maeneo haya.
 
Aidha wajumbe wamekubaliana Mhe. Rais kulihutubia Bunge siku ya Ijumaa jioni kama ilivyokuwa imepangwa awali, ambapo asubuhi kutatanguliwa na shughuli za Mwenyekiti wa Bunge Maalumu kuunda kamati 14 za Bunge Maalum.


 News alert hii imeletwa na 

Owen Mwandumbya Kutoka Sekretariet ya Bunge Maalum
Categories:

Tuesday, March 11, 2014

MWANAMKE AKAMATWA NA MENO YA TEMBO 2 YENYE UZITO WA KILO 15 YA THAMANI YA SHILINGI MILIONI 22








Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari akionesha mbele ya waandishi wa habari Ofisi kwake meno ya tembo vipande 2 yenye thamani ya shilingi 22 hapo jana aliyokamatwa nayo mtuhumiwa Batromeo Mtongwa hapo machi 8 katika kijiji cha kilida katika tarafa ya mamba wilaya ya Mlele ambapo pia mtuhumiwa huyo alikamatwa na gobole 1 na risasi 14.  
Mkazi wa kijiji cha kilida tarafa ya mamba wilaya ya mlele, Patromeo Mtongwa (58) akiwa katika kituo cha polisi cha mkoa wa Katavi  baada ya kukamatwa na meno mawili ya tembo yenye uzito wa kilo 15 yenye thamani ya shilingi milioni 22 na gobole moja pamoja na risasi 14 mtuhumiwa alikamatwa hapo machi 7 mwaka huu majira ya saa mbili usiku nyumbani kwake katika kijiji cha kilida.


Na Walter Mguluchuma Mpanda  Katavi
Mtu mmoja  aliyefahamika  kwa jina la  Bathromeo  James  Mtongwa  58Mkazi wa Kijiji  cha Kilinda Tarafa  ya Mamba  Wilaya  ya Mlele Mkoa wa Katavi  amekamatwa akiwa nameno vipande viwili  vyenye uzito wa kilo 15  vyenye thamani ya shilingi milioni 22 pamoja na Bunduki moja aina ya Gobore na Risasi 14
 
Kwa  mujibu wa Kamanda wa Jeshi la Polisi  wa Mkoa wa Katavi Kamishina  mwandamizi msaidizi  mtuhumiwa  huyo alikamatwa  hapo  machi  7 mwaka huu majira ya saa mbili  na nusu usiku
 
Alisema mtuhumiwa alikamatwa kufutia taarifa ambazo ambazo zililifikia jeshi la polisi  pamoja na askari  wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi kupata taarifa   kuwa mtuhumiwa  anamiliki nyara za Serikali  kinyume  cha sheria  ambapo  taarifa hizo zilipatikana   hapo  machi 6 kutoka kwa Raia wema 
 
Alifafanua ndipo siku hiyo ya tukio majira ya saa mbili usiku polisi wakiwa na Askari wa Hifadhi ya Taifa ya  Katavi  walifika  kwenye kijiji  hicho cha Kilinda  nyumbani kwa mtuhumiwa  Batromeo  na kufanya  upekuzi  nyumbani kwa mtuhumiwa  na kufanikiwa  kukamata risasi 14 
 
Kidavashari alieleza  wakati askari hao wakiendelea na upekuzi kwa kushirikiana na  uongozi wa kijiji    walilitilia shaka eneo moja  la nyumba hiyo  ya mtuhumiwa  kutokana na  eneo hilo kuonekana  kuwa limechimbwa
Alisema ndipo askari walipoamua kuchimba eneo hilo  na baada ya kufukua kwa kitambo kidogo  walifanikiwa  kukuta meno ya Tembo vipande viwili vyenye uzito wa kili 15 yenye thamani ya shilingi milioni 22 yakiwa yamefukiwa ardhini  kwenye shimo 
 
Baada ya kukamatwa kwa  maneno hayo ya Tembo  polisi walianza kumhoji mshitakiwa  kwa kumtaka awaelekeze sehemu ambayo amekuwa akiifadhi  Silaha ambayo amekuwa akiitumia kwenye matukio ya  ujangili
Kidavashari  alieleza baada ya mahojiano mtuhumiwa  aliweza kueleza kuwa bunduki ambayo amekuwa akiitumia kwenye matukio ya ujangili ameifisha  kwenye eneo  linaloitwa King’anda lililopo  ndani ya Hifadhi ya Taifa  ya Katavi
 
Alisema siku ya   tarehe 8 machi   majira ya saa  nane  mchana  mtuhumiwa  aliwaongoza  Askari Polisi  na Askari wa Hifadhi ya Taifa  ya Katavi  na kuwapeleka  katika eneo la King’anda  ndani ya Hifadhi ya Katavi  na  aliweza kuwaonyesha silaha hiyo Bunduki  aina ya Gobore ikiwa imeifadhiwa  kwenye kichaka
 
Mtuhumiwa  anatarajiwa  kufikishwa  Mahakamani  wakati wawote  mara baada ya  upelelezi wa tukio hili utakapo kuwa umekamilika  mapema iwezekanavyo  pia jeshi la polisi Mkoa wa Katavi  lanatowa wito kwa wananchi  kuendelea  kutoa  ushirikiano kwa jeshi la polisi  kwa kutowa taarifa za watu wanaojihusisha  na uwindaji haramu  wa rasilimali za Taifa ili kulinda  na kuhifadhi   rasilimali  zetu  kwa manufaa ya vizazi  vijavyo

“BABU SEYA ALIBAMBIKIWA KESI”….MABERE MARANDO


Nguza Vicking ‘Babu Seya’ na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’.
Marando: Kuna rafiki yangu alikuja kuniomba nifanye kazi ile, nilikataa hasa kwa kuwa nami nina watoto wa kike. Baadaye nilikubali kwanza kusoma jalada la kesi lenye kurasa 1,362 nikaona hawakufanya makosa waliyoshitakiwa, walibambikiwa nikaamua kuwatetea katika ngazi ya rufaa, niliwatetea bure kabisa.
Mwandishi: Kama hivyo ndivyo, ina maana makosa walibambikiwa?
Marando: Ndiyo, naamini makosa yale walibambikiwa lakini siyo na kigogo yeyote wa serikali katika nchi hii. Lakini Mahakama ya Rufaa haina makosa, Babu Seya na wanawe walikuwa wamehukumiwa na magazeti. Nyinyi waandishi mlimhukumu kwa hii fabricated case (kesi ya kutunga) na sababu zipo.
Mwandishi: Je, kuna njia yoyote iliyobaki ya kumtoa Babu Seya na mwanaye?
Marando: Mimi kama wakili, hapo ndiyo mwisho wangu, nimenyoosha mikono. Nimeshindwa nusu, nimeshinda nusu (Kwa kuwatoa jela Mbangu na mdogo wake Francis Nguza na kubaki jela Nguza na Papii.)
Mwandishi: Umekuwa Chadema na kuna habari kuwa uliondolewa kuwa mwanasheria wa chama akapewa Tundu Lissu,pia kuna habari kuwa umekosana na mwenyekiti wako, Freeman Mbowe, Je,  kuna ukweli wowote juu ya hayo?
Marando: Sijawahi kuwa mwanasheria wa Chadema isipokuwa wanapokuwa na tatizo la kisheria huwa nawapa ushauri wakihitaji. Mheshimiwa Mbowe sijakosana naye isipokuwa katika vikao tunaweza kutofautiana na hivyo ndivyo chama makini kilivyo. Wote hamuwezi kuwa na wazo moja katika hoja, baadaye inapigwa kura, upande unaoshinda na unaoshindwa huwa kitu kimoja. Hakuna ugomvi hapo, mimi ni Makamu  Mwenyekiti Kanda ya Pwani na Mjumbe wa Kamati Kuu.
Mwandishi: Lipo suala kuwa wewe ni usalama wa taifa na ulihusika na mauaji ya Komandoo Tamim, Je, hilo unaweza kulifafanua?
Marando: Mimi nilijiunga na usalama wa taifa na nilikuwa kitengo cha mambo ya nje hasa kuhusu vyama vya ukombozi enzi hizo. Niliacha kazi hiyo kwa kukabidhi barua kwa aliyekuwa mkurugenzi wake, Dk. Hansy Kitime baada ya kulazimishwa kujiunga na TANU kwani sikuwa mwanachama. Kuhusu Tamim aliuawa mwaka 1983 wakati huo mimi nilikuwa nimeshaacha kazi.
Hili la kuua walikuwa wakinipakazia watu wa usalama wa taifa bila shaka kwa sababu niliacha kazi kijeuri nikawa jobless (sina kazi).
Baadaye nikaajiriwa Shirika la Sheria Tanzania kabla ya kuanzisha kampuni yangu ya uwakili mwaka 1984. Nimefafanua hili mara nyingi sana, nadhani leo mmenielewa na Watanzania watanielewa.

Kijana Ajichoma kwa Chupa Kichwani Huko Tandika Kisa Maisha Magumu..!!


KIJANA
NI kweli ugumu wa maisha unaweza kumfanya mtu achanganyikiwe na kutamani kujiua ili aondokane na maisha ya duniani?!
Fuatilia mkasa wa kijana huyu, Anord au baba Anjela, mkazi wa Tandika jijini Dar es Salaam ambaye wiki iliyopita aliwashangaza watu waliokuwa katika baa moja iliyopo Davis Corner jijini Dar baada ya kununua bia na kujipiga nayo kichwani, si kwa kufurahisha watu bali kutaka kujiua.
Tukio hilo lilijiri siku ya Jumanne iliyopita ambapo mwandishi wa habari hizi alifika eneo hilo na kufanya mahojiano na mashuhuda kama ifuatavyo:
“Sijui nisemeje! Unajua sisi tulikuwa hapa baa tunakunywa bia huku tukiendelea na maongezi.
“Ghafla huyu kijana alikuja, akanunua bia lakini akaomba isifunguliwe akisema atainywa hivyohivyo. Baada ya muda tukamwona anaipiga kichwani ile chupa hadi ikampasukia kisha akajichomachoma kichwani na shingoni na vipande vyake mpaka damu zikaanza kumtoka kwa wingi.
“Tulishangaa sana. Tena alikuwa akifanya hivyo huku akilia na kusema amechoshwa na ugumu wa maisha, bora ajichome chupa afe ili akapumzike mbinguni ambako hakuna kazi ngumu wala shamba la kulima,” alisema shuhuda huyo.
Anord Akiwa Amelowa Damu
Aliendelea kumweka wazi kijana huyo kwamba, wakati akiendelea kulia alilalamikia kitendo cha kufukuzwa kazi na bosi wake bila hatia huku akitoka mkono mtupu.
“Huku damu zikizidi kumtoka kwa wingi, pia alisema alipofika nyumbani kwake kukawa hakuna chakula cha kulisha familia. Mbaya zaidi siku mbili mbele, mwenye nyumba alifika na kumwambia anataka kodi ya nyumba kama hana ahame,” alisema shuhuda huyo.
Shuhuda akaendelea: “Bila kujali maumivu makali huku damu ikimtoka, jamaa akasema hapa Dar hana ndugu ambaye yupo tayari kubeba mzigo wa familia yake na pia hana fedha ya kurudia kijijini kwao sijui wapi huko. Ndipo aliona bora ajimalize kuliko familia yake kumwona hana msaada wowote.”
Ilielezwa kwamba baada ya tukio hilo na damu zikiwa zimemchafua mwili mzima, kijana huyo alikwenda kwa mhudumu wa baa hiyo na kumtaka amuuzie bia nyingine  lakini alimkatalia akiamini angeendelea kujichoma.
Baada ya kukataliwa, alikwenda kwenye duka la jirani akanunua soda ambayo pia aliipigisha kichwani na kumpasukia.
Inaelezwa kuwa damu zilizidi kumtoka kwa wingi, hakuna mtu aliyemsogelea.
Shuhuda anasema watu walikusanyika, wengine wakapiga simu Kituo cha Polisi Chang’ombe jijini Dar ambapo walifika na kumchukua kwenye ‘difenda’ hadi Hospitali ya Temeke.
KIJANA1
Gari la Polisi Lililomchukua
Habari zinasema baada ya matibabu, kijana huyo akiwa na bandeji kichwani alirudi kwenye baa hiyo na kuomba kuuziwa bia nyingine lakini hakupewa huduma zaidi ya wateja kumshangaa.
Uwazi lilijaribu kuzungumza na kijana huyo lakini hakuwa tayari zaidi ya kuporomosha matusi na kuendelea kulalamikia ugumu wa maisha.

Mahakama yawaruhusu Basil Mramba na Daniel Yona kwenda kutibiwa nje ya nchi….



MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imewaruhusu kwenda kutibiwa nje ya nchi  Mawaziri Waandamizi wa zamani,  Basil Mramba na Daniel Yona wanaokabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia Serikali hasara ya Sh. bilioni 11.7  kwa kutoa msamaha wa kodi baada ya kusikiliza maombi yao leo.
 
Uamuzi huo umetolewa leo mahakamani hapo na Jaji John Utamwa baada ya washtakiwa hao kuwasilisha maombi ya kwenda kutibiwa nje ya nchi.
 
Upande wa Jamhuri ulidai kuwa hauna pingamizi na maombi hayo.
mramba
 
Jaji Utamwa alisema baada ya kusikiliza maombi hayo mahakama inawaruhusu washtakiwa kusafiri kwenda nje ya nchi kutibiwa na kwamba pamoja na ruhusa hiyo Mramba na Yona siku ya kusikiliza kesi Aprili 22, mwaka huu wahudhurie mahakamani.
 
Mbali na Mramba na Yona, mshtakiwa mwingine ni, Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja.
Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa Aprili 22 hadi 25, mwaka huu.
 
Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuwa, kati ya Agosti mwaka 2002 na Juni 14 mwaka 2004 jijini Dar es Salaam, wakiwa watumishi wa umma kama mawaziri na katibu mkuu walitumia vibaya madaraka.
 
Ilidaiwa kuwa kwa kupitia kampuni ya Alex Stewart (ASSAYERS) ya Uingereza iliyoingia mkataba wa ukaguzi wa madini ambapo kwa kupitia kampuni tanzu ya Alex Stewart ( ASSAYERS) Government Business Corporation  waliingia mkataba kukagua kiwango cha uzalishaji wa madini ya dhahabu kinyume cha Sheria ya Manunuzi ya Umma.

TAZAMA PICHA ZA AJALI MBAYA ILIYOTOKEA HUKO SAME MKOANI KILIMANJARO




Wednesday, March 5, 2014

TASWIRA MBALIMBALI KWENYE BUNGE LA KATIBA JANA MJINI DODOMA

 Mjumbe Mhe. Tundu Lissu akitoa ufafanuzi ya moja ya hoja zilizowekwa mezani na wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba wakati wa majadiliano ya rasimu za kanuni
 Mjumbe Mhe Evod Mmanda akijibu hoja
Mjumbe Mhe. George Simbachawene akitoa ufafanuzi. 
Mjumbe wa kamati ya kuandaa rasimu ya kanuni  ambaye pia anatoka kundi la walemavu Mhe. Amon Anastaz Mpanju akijibu hoja za wabunge. 
(Picha na Deusdedit Moshi)
Categories:

PICHA NA HABARI KAMILI YA HOSPITALI ILIVYOJAA MAJI YA MVUA NA KUSITISHA KUTOA HUDUMA ZAKE DAR

Mapema mchana wa leo kumetokea mvua kubwa katika maeneo mbalimbali ya Jijini Dar es salaam, kumesababisha usumbufu mkubwa baada ya maeneo mengi kukumbwa na tatizo la maji mengi ambayo yaliziba barabara , nyumba za watu pamoja na maeneo mbalimbali.

Mvua hizo kubwa ambazo hata mamlaka ya hali ya hewa wametahadhalisha kwamba zitakuwepo kuanzia Tarehe 5.03.2014 hadi Tarehe 7.03.2014  zimesababisha usumbufu mkubwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Kinondoni Sinza - Palestina kujaa maji kila kona na kupelekea wauguzi kuacha kazi na kupanda juu ya Meza na viti wakikwepa maji hayo. Na wengine kukimbia katika eneo hilo kuhofia maji hayo.

Walikwepa maji hayo kutokana na kwamba si ya mvua tuu lakini yalikuwa ni Machafu yaliyochanganyikana na maji kutoka vyooni ambapo kuna chemba moja ya maji machafu imepita hapo.

Baada ya mvua hiyo kwisha iliwalazimu wafanya usafi wachukue muda wa zaidi ya dakika 30 kufanya usafi na kutoa matope yaliyokuwa yamejaa kila chumba.

Akiongea kwa Simu Mganga Mkuu wa Hospitalu hiyo amekili kwamba kuna usumbufu mkubwa wa chemba hiyo na mvua hasa katika kipindi hicho ambapo zinanyesha kwa kiasi kikubwa. 

Ameongeza kwa kusema kwamba kunajuhudi zinahitajika kufanyika ili kuweza kunusuru tatizo hilo lisiendelee.
Nao baadhi ya wagonjwa ambao wengine walikuwa katika hali ambayo si nzuri wamesema  wanaiomba serikali itazame tatizo hilo maana licha ya maji hayo kuwa mengi lakini pia ni hatari kwa afya zao kwa ujumla.

Hii ndio picha halisi ilivyokuwa katika picha hizi..
 Huu ni mtaro wa kupitisha maji taka ambao umepita kati kati ya Hospitali ya Palestina amapo ulifumuka na kusababisha kusambaa kwa maji machafu katika kila kona ya Hospitali hiyo
 Mmoja wa wagonjwa akiwa anangojea kupata huduma baada ya mvua hiyo kubwa kwisha
 Haya ni maji machafu ambayo yametapakaa kila sehemu ya hospitali
 Kushoto ni Mgonjwa akiwa amelala juu ya Benchi ambapo pembeni kuna maji na matope ambayo yamechanganyikana na kinyesi kutoka katika vyoo mbalimbali katika makazi ya watu.
 Hii ndio hali halisi ya Chemba hii ambayo ipo ndani ya Hospitali ya  Sinza Palestina
 Hizi ni chemba zaidi ambazo zipo nje na pia zimeungana na zilizopo ndani ya Hospital hiyo
 Wagonjwa zaidi wakingojea waganga kufika pia kumalizia kusafishwa kwa vyumba hivyo ili wapate hudumiwa
 Moja ya Chumba ambacho kilikuwa kimejaa tope kikingojea kusafishwa
 Hapa hata hapapitiki
 Baadhi ya viti vikiwa vimeegeshwa kwa ajili ya kungoja kufanya usafi
 Hakuna mtu katika maeneo haya kutokana na mvua kubwa iliyonyesha

 Kila kitu kimekaa hovyo hovyo baada ya mvua kubwa hiyo kunyesha
 Baadhi ya vifaa vya kutibia wagonjwa vikiwa juu ya moja ya kitanda cha kutibia wagonjwa huku watu wakingoja huduma ya matibabu.
 Huu ndio Mtaro wa maji machafu ambapo maji kutoka nje yamepita ndani ya hospitali hiyo na kusababisha maafa baada ya Mtaro huo kuziba. Picha zote na Dar es salaam yetu.