Wednesday, June 4, 2014

UKATILI: Kichanga chaokotwa ndani ya SHIMO huko Jijini Mbeya..!!

WIMBI la wanawake mkoani Mbeya kujifungua watoto na kisha kuwatupa na wengine kutoa mimba limezidi kushika kasi na kukithiri baada ya vitendo hivyo kuripotiwa na vichanga kuokotwa kwenye mashimo na mitoni.
Kukithiri kwa vitendo ni baada ya leo Wananchi wa Mtaa wa Mwambenja kata ya Iganzo jijini Mbeya kugundua kutupwa kwa mtoto anayesemekana kuwa na umri usiozidi siku moja jinsia ya kike katika shimo la choo kisichotumika.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa Mtaa huo, aliyefahamika kwa jina la Lukasi Mwakalonge, alisema alipewa taarifa na wananchi wake mchana na kuambiwa kuna katoto kametupwa shimoni na bado ni kazima hali iliyomlazimu kutoa taarifa katika Jeshi la Polisi.
Alisema baada ya kufika eneo la tukio na kugundua kuwa mtoto bado yuko hai wakaamua kumtoa ndani ya shimo huku wakisubiri jeshi la polisi kwa ajili ya hatua zaidi lakini akawa amepoteza maisha muda mfupi baada ya kutolewa ndani ya shimo.
Kichanga kikiwa kimefunikwa Baada ya kuokolewa na muda mchache kufariki
Kichanga kikiwa kimefunikwa Baada ya kuokolewa na muda mchache kufariki
Shimo ambamo kichanga hicho kimekutwa
Shimo ambamo kichanga hicho kimekutwa
Mashuhuda wakishuhudia
Mashuhuda wakishuhudia
Wengine wakiwa wameduaa
Wengine wakiwa wameduaa
Watoto wakiwa wanatimuliwa eneo la tukio
Watoto wakiwa wanatimuliwa eneo la tukio
Watoto wakiwa wanatimuliwa eneo la tukio
Watoto wakiwa wanatimuliwa eneo la tukio
Hata hivyo jeshi la Polisi lilifika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu, vitendo hivyo vya wanawake kutupa watoto kabla na baada ya kujifungia bado vinazidi kutokea hapa nchini ingawa hakuna takwimu sahihi za wanawake waliopatikana na hatia kwa makosa kama hayo.

No comments:

Post a Comment