Wednesday, April 30, 2014

KATIBU MKUU WA FIFA KUWASILI NCHINI LEO

SERIKALI NA WAASI WA SUDAN KUSINI WADAIWA KUWATUMIA WATOTO VITANI

RAIS JK ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA MKUU WA MKOA WA SINGIDA KUFUATIA AJALI ILIYOUA WATU 19

IGP, DCI WALA KIAPO CHA KUWA WAJUMBE WA TUME YA UTUMISHI YA JESHI LA POLISI NA MAGEREZA




DC NJOMBE AWATAKA WAZAZI KUWASILISHA CHAKULA KWA AJILI YA WANAFUNZI SHULENI


 
Mkuu wa wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba
 
Na Michael Ngilangwa
 
Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba amelejea tena kusisitiza kauli ya serikali ya kuwataka wazazi na walezi kuchangia chakula shuleni pamoja na kuwakamilishia mahitaji mbalimbali ya shule  ili kuwepo kwa mahudhurio mazuri ya wanafunzi na kuboresha kiwango cha taaluma.


Akizungumza na mtandao huu Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba ameziagiza kamati na bodi za shule mbalimbali zilizopo katika halmashauri  Ya Wilaya ya Njombe kuhakikisha zinasimamia ujenzi wa miundombinu  ya vyoo huku wazazi wakitakiwa kuwanunulia  mahitaji ya shule na kuwaweka watoto katika mazingira ya usafi.


Aidha bi.Dumba amesema kuwa katika ziara zake za kutembelea maeneo mbalimbali wilayani Njombe kukagua utekelezaji wa miradi  amebaini kuwepo kwa tatizo la baadhi ya shule kukosa huduma za chakula,wanafunzi kutokuwa na sale za shule pamoja na kukosekana kwa vyoo bora kwa maeneo yote ya shuleni na nyumbani.


Amesema kuwa kukosekana kwa huduma bora za vyoo zinaweza kusababisha mripuko wa magonjwa katika maeneo ya shule na nyumbani ambapo amewataka wataalamu wa afya wa kata na vijiji  kutembelea maeneo hayo ili kukagua na kuhimiza usafi wa mazingira  katika maeneo ya shule na makazi ya wananchi na kujikinga na mlipuko wa magonjwa hayo Huku kamati na bodi akizitaka kupeleka miundombinu ya maji kwa kushirikiana na wananchi ili vyoo  viweze kutumia maji.


Katika hatua nyingine Bi.Dumba amewataka wananchi kuepukana na unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na kwamba  hatua kali zinatakiwa kuchukuliwa kwa baadhi wanaoendekeza tabia hiyo ikiwa ni pamoja na kuwanyanyasa watoto huku akiwataka viongozi wa serikali za vijiji na kata kudhibiti tabia hiyo isiendelee kwani ni kitendo cha kumkandamiza mwanamke na mtoto.
 

MKURUGENZI WA HABARI ATOA UFAFANUZI TUZO YA JAJI WARIOBA

Na Magreth Kinabo, Maelezo
Mkurugenzi  wa Idara  ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene amesema Jaji Joseph Warioba alitunukiwa tuzo ya muungano iliyotukuka   kwa kuwa alistahili kupewa kama viongozi wengine na  kuwa kitendo si kumkejeli kama baadhi ya vyombo vya habari vilivyoripoti  hivi karibuni.
Hayo yalisemwa leo na Mkurugenzi huyo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu  suala hilo katika  mkutano na waandishi wa habari uliofanyika  kwenye Ukumbi wa  MAELEZO jijini Dares Salaam.
“Kumekuwa kuna taarifa katika baadhi ya magazeti kuwa Serikali kumpa tuzo Jaji Warioba ni kumkejeli, Ninapenda kuwataarifu kuwa  kitendo cha Serikali kumpa tuzo Jaji Warioba haikumkejeli wala kumtukana. Jaji Warioba anastahili kupewa tuzo kama mawaziri wakuu wengine kwa kuwa mchango wake katika muungano unajulikana,” alisema Mwambene. 
Tuzo hiyo aliyoipewa Jaji Warioba, wakati wa maadhimisho ya mika 50 ya Muungano wa Tangayika na Zanzibar.
 Mwambene aliongeza kuwa  tuzo hiyo haihusiani na mjadala wa  Rasimu ya Katiba. Alifafanua kuwa katika mjadala wa Sura ya Kwanza na ya Sita ya Rasimu ya Katiba uliokuwa ukifanyika katika Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma, baadhi ya wajumbe walikuwa wanatoa mawazo yao na si kwamba wanapingana na Jaji Warioba. 
“ Mjumbe anatoa mawazo yake wakati wa kujadili  kwa kuwa hiyo bado ni rasimu, hivyo  hapingani  na Jaji Warioba,” alisisitiza huku akisema rasimu huwa inafanyiwa marekebisho.
Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo , alisema bado Ofisi yake inaendelea na hatua ya pili kuhusu gazeti la MAWIO kutoa maelezo ya kuchapisha habari yenye kichwa cha habari ‘Hati  Muungano Utata’.
Mwambene alifafanua kuwa ofisi hiyo inaendelea na suala hilo kwa hatua hiyo ili kutoa nafasi kwa viongozi husika wa gazeti  kutoa maelezo baada ya hapo awali  kupeleka  barua ya kutaka maelezo hayo kwenye Ofisi za  gazeti la ‘MAWIO’ na kukuta zimefungwa.
 Aidha alisema kuwa hata majirani wa ofisi hizo walikataa kupokea barua hiyo, kwa maelezo kuwa kama ni masuala  ya habari  wahusika ndio wanapaswa kuipokea.
Aliongeza kwamba ofisi yake itafanya maamuzi sahihi ikiwahaitapata maelezo hayo, hivyo isijeikalaumiwa.
Mwambene aliwataka waandishi wa habari kuwa na kitambulisho  cha  uandishi wa habari (Press Card) na ametoa muda wa wiki moja kuanzia leo kwa mwandishi ambaye hana ili kuweza kukamilisha taratibu za kukipata.
Pia amewataka waandishi wa habari kuwa na heshima  katika utendaji kazi wa taaluma hiyo na kuzingatia mavazi yanayostahili kwani wao ni kioo cha jamii.

Lishe asili ni dawa ya wagonjwa wa moyo

140430034802_kula_vyakula_asili_inazidisha_miaka_ya_wagonjwa_wa_moyo_512x288_bbc_nocredit_c9f25.jpg
 Wanasayansi nchini Marekani wanasema watu waliowahi kupata maradhi ya moyo wanaweza kuishi maisha marefu iwapo watakula zaidi vyakula ambavyo havijapitia viwandani.
Watafiti walichunguza zaidi ya watu elfu nne waliowahi kupata mshituko wa moyo na kubaini kuwa wana uwezekano mkubwa wa kuishi miaka tisa zaidi kama watakula vyakula hivyo .
Vyakula ambayo havijapitia viwandani vina nyuzinyuzi ambazo tayari imethibitishwa kuwa husaidia katika kuwezesha binadamu kwenda haja bila matatizo.
Vyakula ambayo vina nyuzinyuzi hizo ni kama vile matunda, mboga na nafaka.
Hatahivyo wataalam wanasema watu katika mataifa mengi hawali vyakula hivyo kwa wingi.CHANZO BBC

Ronaldo avunja rekodi ya Messi

140429194121_cristiano_ronaldo_real_madrid_512x288_afp_nocredit_79dc4.jpg
 Nyota wa Real Madrid ya Uhispania Cristiano Ronaldo amevunja rekodi ya Lionel Messi ya ufungaji mabao mengi zaidi katika ligi ya mabingwa barani Uropa alipoifungia timu yake mabao mawili na kuisaidia kuichapa Bayern Munich mabao 4-0 katika nusu fainali jana usiku
Mreno huyo mwenye umri wa miaka , 29,alifunga bao lake la 15 na 16 msimu huu katika uwanja wa Allianz Arena.
Kufuatia ushindi huo Real Madrid ilifuzu kwa fainali ya mchuano huo kwa jumla ya mabao 5-0.
Ronaldo sasa amefunga mabao 16 katika mechi kumi za ligi hiyo ya mabingwa Barani Ulaya mbili zaidi ya Lionel Messi wa Barcelona .
Rekodi hiyo ya mabao 14 ilikuwa ikishikiliwa kwa pamoja kati ya Messi (2011-12, Barcelona), Ruud van Nistelrooy (2002-03, Manchester United) na Jose Altafini (1962-63, AC Milan).
Kwa jumla Ronaldo amefunga mabao 67 katika ligi hiyo ya mabingwa barani ulaya sawa na Messi na ni mabao manne tu nyuma ya rekodi ya idadio kubwa zaidi ya mabao yaliyofungwa na mchezaji wa zamani wa Real na Schalke Raul.CHANZO BBC

Thursday, April 17, 2014

Real Madrid ni mabingwa wa Copa del Rey

REAL_e7e7c.jpg
Timu ya Real Madrid ndio mabingwa wa mwaka huu wa kombe la Copa del Rey .
Madrid waliwacharaza wapinzani wao wa jadi katika ligi ya nyumbani La liga Barcelona mabao 2 kwa 1 katika fainali iliyochezwa jana mbele ya mfalme wa Uhispania .
Kocha wa Madrid Carlo Ancelotti alikuwa anajikuna kichwa kwani mshambulizi wake nyota Cristiano Ronaldo hakuwa uwanjani kutokana na jeraha la mguu na hivyo ikambidi kumchezesha mshambulizi aliyegharimu kitita kikubwa
zaidi msimu huu Gareth Bale .
Na alidhibitisha udedea wake alipofuma bao la ushindi zikiwa zimesalia dakika tano tu mechi hiyo kukamilika na hivyo kuisadia kutwaa taji lake la 19 la Kombe hilo la mfalme la Copa del rey.
Real Madrid ilidhibitisha niya yao mapema kwa bao la dakika ya 11 Angel Di Maria
madre_dcf63.jpg
Lakini ikasawazishwa na bao la Bartra katikadakika ya 68 ya kipindi cha pili.
Bao la ushindi lilifungwa na Gareth Bale dakika tano tu kabla ya mechi hiyo kukamilika .
Bale alitimuka mbio na kumpiku mlinzi wa Barca Marc Bartra katikati ya kiwanja na akafululiza hadi akampiga chenga kipa machachari Jose Manuel Pinto na kuihakikishia Madrid ushindi.
Real Madrid bado iko mbioni kuwania kombe la ligi ya Uhispania, ambapo inashikilia nafasi ya pili na alama 79 alama tatu nyuma ya wakinzani wao Athletico Madrid.
Barcelona ambayo imekuwa ikishuhudia msururu wa matokeo yasiyo ya kuridhisha katika siku za hivi punde inafunga orodha ya tatu bora ikiwa na alama 78.
Madrid sasa inamuda wa kutoka kujiandaa kwa mechi ya nusu fainali ya kombe la mabingwa barani Ulaya dhidi ya mabingwa watetezi Bayern Munich ya Ujerumani.
Mechi nyingine ya nusu fainali ya kombe la mabingwa barani Ulaya itakuwa kati ya Chelsea ya Uingereza dhidi ya Atletico Madrid.
Nusu fainali hizo zitachezwa juma lijalo.

Angalia Yanayojiri katika Bunge Maalum la Katiba-Dodoma

kamati_af0f6.jpg
Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Bunge Maalum la Katiba wakiwa katika kikao cha Kamati hiyo leo mjini Dodoma, kilichokuwa kikijadili mambo mbalimbali ikiwemo jinisi ya kuwasaidia waathirika wa mafuriko yaliyotokea hivi karibuni.
sitaa_e5cc8.jpg
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samuel Sitta(kushoto) akiongoza kikao cha Kamati ya Uongozi wa Bunge hilo  leo mjini Dodoma wakati wakijadili mambo mbalimbali ikiwemo jinisi ya kuwasaidia waathirika wa mafuriko yaliyotokea hivi karibuni. Kulia ni Katibu wa Bunge hilo Yahya Khamis Hamad.


pundu_ec740.jpg
Mjumbe wa Kamati ya Uongozi ya Bunge Maalum la Katiba Pande Ameir Kificho akitoa mchango wake wakati wa kikao cha Kamati hiyo leo mjini Dodoma, kilichokuwa kikijadili mambo mbalimbali ikiwemo jinisi ya kuwasaidia waathirika wa mafuriko yaliyotokea hivi karibuni.

Katiba, naye Shaaaban Robert kwenye kitabu chake cha ' Kufikirika' anasema...

9789976973068_964e9.jpg
" Mtoto wa Mfalme wetu ni mgonjwa kitandani. Mikoba ya waganga wetu wote bora imemiminia dawa zote zilizokuwamo ndani yake. Haikutokea hata dawa moja kuwa mujarabu. Hatari ya maisha ya mtoto inahofiwa sana. Mfalme astahili msaada wa kila raia. Wanatakiwa watu wawili; mwerevu na mjinga, kwa kafara. Idhini ya Baraza hili yatafutwa. Heshima kubwa kama hii bado kutokea. Idhini ikipatikana kafara litafanywa mara moja. Inatazamiwa kuwa salama ya mtoto wa Mfalme imetegemea Baraza hii. Tumepewa fahari ambayo nchi yo yote ulimwenguni bado kuwapa washauri wake."- Shaaban Robert

MAGAZETI YA LEO IJUMAA

0_78767.jpg
01_8031b.jpg
1_be432.jpg
02_d06bd.jpg
2_c65d0.jpg
3_2de63.jpg
4_dd3c4.jpg
5_55385.jpg
6_d2280.jpg
7_3ebd6.jpg
8_2e738.jpg
9_8bfb0.jpg
10_d9398.jpg
11_56bcc.jpg
12_1505f.jpg
13_1180d.jpg
014_0cbc1.jpg
14_58109.jpg
15_cc029.jpg
16_4eff7.jpg
017_1_03d3a.jpg
017_3_102b1.jpg
017_4_63320.jpg
017_5_65012.jpg
017_6_eb8f1.jpg
017_7_8663f.jpg
17_15d89.jpg
IMG-20140418-WA0009_05c28.jpg
IMG-20140418-WA0010_cb156.jpg
  IMG-20140418-WA0011_b2bf0.jpg
IMG-20140418-WA0013_dec76.jpg
IMG-20140418-WA0014_560e2.jpg
IMG-20140418-WA0039_ee743.jpg
IMG-20140418-WA0041_44ee1.jpg