Sunday, August 24, 2014

Taarifa ya kufungwa kwa kipande cha barabara ya Mandela-Ubungo

kielelezo

Mkandarasi Mkuu anayeshughulikia mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam, Strabag International ametangaza kufungwa kwa muda kipande cha barabara ya Mandela hadi makutano ya Ubungo Mataa.

Ofisa Uhusiano wa kampuni hiyo Bw. Yahya Mkumba amesema kipande cha barabara ya Mandela kuanzia makutano ya barabara ya Morogoro upande wa kushoto uelekeo wa Tabata kuanzia Ubungo Mataa hadi Darajani patafungwa kuanzia tarehe 25/08/2014 mpaka tarehe 30/08/2014 ili kupisha ujenzi.
Watumiaji wa barabara hiyo watalazimika kutumia upande mmoja wa barabara hiyo. Magari yatakayokuwa yanatokea Mwenge, Kimara na Shekilango yatalazimika kutumia barabara ya upande wa kulia ambayo pia itakuwa ikitumika na magari yanayotoka Tabata kuelekea Ubungo.

“Tunaomba radhi kwa usumbufu utakaotokea,” alisema Bw. Mkumba.

Magazeti Leo Jumatatu

1_20fa8.jpg
2_05cb9.jpg
03_d1b5b.jpg
3_ce702.jpg
4_275ee.jpg
5_9a843.jpg
004_80ae6.jpg
04_5deb2.jpg
10_f3ddb.jpg
11_0b372.jpg
20_db4bf.jpg
22_267d1.jpg
23_192a9.jpg
00024_2551c.jpg
0024_87bee.jpg
24_5abbd.jpg
25_0f057.jpg
26_a4479.jpg
27_ee699.jpg
28_8bf48.jpg
29_ead1b.jpg
30_bbbfd.jpg
31_b213d.jpg
35_458b0.jpg
36_d7a07.jpg
40_3b18f.jpg
41_7e9b9.jpg
42_c0e27.jpg

Tuesday, July 22, 2014

MKE WA POLISI AFIA NYUMBANI KWA MWENDESHA BODABODA


Jeshi la Polisi linamshikilia dereva mmoja wa pikipiki, maarufu kama bodaboda wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro baada ya mke wa askari polisi kukutwa amekufa chumbani kwa dereva huyo. 
 
Tukio hilo ambalo limezua gumzo kubwa wilayani humo lilitokea juzi saa 12:00 jioni katika eneo la New Mwanga wilayani humo na mtuhumiwa akidaiwa kukutwa akiwa amelewa chakari.
 
Mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Shaibu Ndemanga amethibitisha kuwapo kwa tukio hilo na kusema uchunguzi unaendelea.
 
“Hilo tukio lina ukweli na bahati mbaya sana mumewe ndiyo kwanza amehamishiwa Geita na alikuwa akaripoti halafu aje kuchukua familia yake,” alisema Ndemanga.
 
Mkuu huyo wa wilaya ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo, alisema hadi sasa haijafahamika nini kilitokea na kwamba hilo ni moja kati ya mambo ambayo polisi inachunguza.
 
“Hayo yote kwamba ilikuwaje akawa chumbani kwa huyo kijana, nini sababu za kifo yatajulikana kadiri upelelezi unavyoendelea,” alisema.
 
Imeelezwa kuwa jana ilikuwa siku ya askari huyo kuripoti katika kituo chake kipya cha kazi.
 
“Mpaka sasa hivi haijajulikana nini hasa kilitokea huko chumbani na ilikuwaje akawa chumbani kwa huyo dereva,” alisema mmoja wa watu waliokuwapo katika eneo la tukio ambaye hata hivyo, hakutaka kutaja jina lake na kuongeza kuwa jana saa sita mchana, mwili wa mwanamke huyo ulichukuliwa kutoka Hospitali ya Wilaya ya Mwanga na kuhamishiwa Hospitali ya Rufaa ya KCMC kwa uchunguzi.
 
Taarifa za awali zinasema kuwa mwili wa marehemu ulikuwa na mikwaruzo shingoni hali inayotia shaka kuwa huenda alinyongwa.
 
Habari nyingine zinadai kuwa siku ya tukio, mwanamke huyo alikuwa ameaga kuwa anakwenda kanisani lakini baadaye simu yake ilipopigwa ilikuwa ikipokewa na mwanamume.
 
Ilidaiwa kuwa mume wa marehemu alipojaribu kupiga simu ya mkewe, ilikuwa ikipokelewa na mtu aliyeonekana kuwa ni mlevi wa kupindukia hali iliyomtia wasiwasi na kuamua kuwapigia simu marafiki zake wa karibu ili wamsaidie kumtafuta ndipo walipopata taarifa kuwa ulikuwapo uhusiano kati ya shemeji yao na dereva huyo wa bodaboda.
 
Ilidaiwa kuwa marafiki hao walikwenda moja kwa moja nyumbani kwa dereva huyo wa bodaboda ambako walimkuta akiwa amelewa na walipoingia ndani walimkuta shemeji yao akiwa ameshafariki dunia.

Kamanda wa Polisi Mkoa Kilimanjaro, Robert Boaz hakupatikana jana kuzungumzia tukio hilo kwa kuwa alikuwa kwenye ziara ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda huko Gonja wilayani Same. 

Credit: Mwananchi

WAKAMATWA WAKIWA NA MABOMU 7 RISASI 6 NA BARUTI JIJINI ARUSHA



JESHI la polisi hapa nchini limefanikiwa kuwatia mbaroni vinara wa milipuko ya mabomu hapa nchini, Yusufu Ally (30) na mkewe Sumaina Juma (19), wakazi wa Sombetini, wakiwa na mabomu ya kurusha kwa mkono aina ya Gurnet saba, risasi sita za shotgun, baruti, mapanga mawili na bisibisi moja. 

Mtaalamu wa mabomu kutoka Jeshi la Polisi akionyesha kwa waandishi wa habari moja ya bomu lililokamatwa.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Isaya Mngulu, alisema kati ya mabomu hayo moja limetengenezwa nchini Ujerumani na sita yametengenezwa Urusi.
 
Alisema watuhumiwa hao walikamatwa jana saa 2 usiku katika eneo la Sombetini mjini hapa baada ya jeshi la polisi kupata taarifa juu ya watuhumiwa hao kuhusika na matukio ya milipuko ya mabomu.
 

 
Aliongeza kuwa polisi inamtafuta kinara muhimu wa mabomu, Yahaya Hussen Hela (35), mkazi wa Mianzini jijini hapa, huku watuhumiwa wengine 25 akiwemo mfanyabiashara maarufu jijini hapa anayemiliki mabasi ya Kandahal Said Temba (42), pamoja na Imamu wa Msikiti wa Masjidi Qubia, Japhal Lema (38) ambaye pia ni mwalimu wa shule ya msingi wilayani Arumeru wakishikiliwa kuhusisana  matukio ya mabomu.
 
Miongoni mwa watuhumiwa hao, sita kati yao wanahusishwa na tukio la ulipuaji wa mgahawa wa Vama uliotokea Julai 7, mwaka huu,na kusababisha majeruhi wanane raia wenye asili ya Kiasia.
 

Watuhumiwa sita wa mlipuko huo wametajwa kuwa ni Shabani Hussen (38)ambaye alikuwa mlinzi katika mgahawa huo, Mohamed Nuru (30) mlinzi wa mgahawa wa jirani na tukio, Japhari Lema (38), Abdul Mohamed (31), wakala wa mabasi stand pamoja na Said Temba (42), wote wakazi wa jijini Arusha.
 
Mngulu alisisitiza kuwa polisi inaendelea kuwasaka wahuhumiwa wengine zaidi na kwamba jeshi hilo limeahidi kutoa zawadi kwa atakayeweza kutoa taarifa za siri zitakazowezesha kupatikana kwa wahusika hao.


Credit: Global publisher.

Wednesday, June 4, 2014

UKATILI: Kichanga chaokotwa ndani ya SHIMO huko Jijini Mbeya..!!

WIMBI la wanawake mkoani Mbeya kujifungua watoto na kisha kuwatupa na wengine kutoa mimba limezidi kushika kasi na kukithiri baada ya vitendo hivyo kuripotiwa na vichanga kuokotwa kwenye mashimo na mitoni.
Kukithiri kwa vitendo ni baada ya leo Wananchi wa Mtaa wa Mwambenja kata ya Iganzo jijini Mbeya kugundua kutupwa kwa mtoto anayesemekana kuwa na umri usiozidi siku moja jinsia ya kike katika shimo la choo kisichotumika.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa Mtaa huo, aliyefahamika kwa jina la Lukasi Mwakalonge, alisema alipewa taarifa na wananchi wake mchana na kuambiwa kuna katoto kametupwa shimoni na bado ni kazima hali iliyomlazimu kutoa taarifa katika Jeshi la Polisi.
Alisema baada ya kufika eneo la tukio na kugundua kuwa mtoto bado yuko hai wakaamua kumtoa ndani ya shimo huku wakisubiri jeshi la polisi kwa ajili ya hatua zaidi lakini akawa amepoteza maisha muda mfupi baada ya kutolewa ndani ya shimo.
Kichanga kikiwa kimefunikwa Baada ya kuokolewa na muda mchache kufariki
Kichanga kikiwa kimefunikwa Baada ya kuokolewa na muda mchache kufariki
Shimo ambamo kichanga hicho kimekutwa
Shimo ambamo kichanga hicho kimekutwa
Mashuhuda wakishuhudia
Mashuhuda wakishuhudia
Wengine wakiwa wameduaa
Wengine wakiwa wameduaa
Watoto wakiwa wanatimuliwa eneo la tukio
Watoto wakiwa wanatimuliwa eneo la tukio
Watoto wakiwa wanatimuliwa eneo la tukio
Watoto wakiwa wanatimuliwa eneo la tukio
Hata hivyo jeshi la Polisi lilifika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu, vitendo hivyo vya wanawake kutupa watoto kabla na baada ya kujifungia bado vinazidi kutokea hapa nchini ingawa hakuna takwimu sahihi za wanawake waliopatikana na hatia kwa makosa kama hayo.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI


1 74c6e
01 96e6d
02 4e893
2 8c0b6
3 b0699
4 738a9
5 d3f2a
6 6c494
7 d9c86
35 1236a
36 21db2
37 1d757
38 88c85
39 07c88
40 ac389
050 20284
51 a0a9f
52 c0c0e
53 ff5d7
54 1cc07
55 3eca4
56 ea54a
60 92ef1
61 cda74
62 b4d38
63 b795f
64 d7bf4
65 f239f