Wednesday, February 26, 2014

SHEIKH PONDA AGONGA MWAMBA TENA MAHAKAMANI, DPP AWEKA PINGAMIZI

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), ameendelea kuweka pingamizi dhidi ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania, Sheikh Issa Ponda akipinga maombi yake ya kufanya marejeo ya uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro. 
 
Sheikh Ponda anakabiliwa na kesi ya jinai katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, akidaiwa kufanya uchochezi maeneo mbalimbali mkoani humo na kukaidi amri ya Mahakama ya Kisutu ya Mei 9, mwaka jana ya kumtaka kuhubiri amani kwa jamii likiwa ni sharti la kifungo cha mwaka mmoja nje.
 
Awali, Sheikh Ponda aliomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro imfutie shtaka hilo la kukaidi amri ya Mahakama ya Kisutu, lakini Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro ilimkatalia, aliamua kuwasilisha maombi Mahakama Kuu akiiomba ifanye marejeo ya uamuzi huo.
 
Hata hivyo, maombi hayo yalitupiliwa mbali Desemba 11, mwaka jana baada ya DPP kumwekea pingamizi kuwa hati ya kiapo iliyokuwa ikiunga mkono maombi yake, ilikuwa na kasoro za kisheria kwa kuwa haikuwa ikitimiza matakwa ya Sheria ya Viapo kwa kutokuonyesha jina la aliyeapa na tarehe.
 
Baada ya kutupiliwa mbali, Wakili wa Ponda, Juma Nassoro aliwasilisha tena maombi hayo.
 
mahakamani hapo baaada ya kufanya marekebisho ya kasoro hizo za kisheria.
 
Maombi hayo mapya yalipangwa kusikilizwa jana na Jaji Augustine Mwarija, lakini yalikwama baada ya DPP kuwasilisha tena pingamizi la awali akiiomba mahakama iyatupilie mbali akidai kuwa yamewasilishwa kinyume na kifungu cha 372 (2) Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA).

MAGARI YATEKWA ABIRIA WAPEWA KICHAPO BARABARA YA MBEYA - NJOMBE

WATU wasiofahamika majina wala makazi yao, juzi walifunga Barabara Kuu ya Mbeya-Njombe, Wilaya ya Mbarali, mkoani Mbeya kwa kuweka mawe, magogo, kuteka magari na kujeruhi abiria waliokuwa katika magari hayo.

 Akizungumza na waandishi wa habari mjini Mbeya jana, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo, Robert Mayala, alisema tukio hilo lilitokea saa 1:30 usiku, Kijiji cha Machimbo, Kata ya Rujewa.

Alisema watu hao walikuwa na silaha za jadi kama mapanga, rungu, mawe na fimbo ambapo katika tukio hilo, baadhi ya abiria walijeruhiwa na kuporwa vitu mbalimbali.

Vitu hivyo ni pamoja na pesa taslimu, simu za mkononi na mikoba ambayo thamani yake wala idadi haijafahamika.
 
"Hawa watu waliwashambulia baadhi ya abiria kwa kuwapiga sehemu mbalimbali za miili yao kwa kutumia silaha ambazo walikuwa nazo, kufanya uharibifu katika baadhi ya magari kwa kuvunja vioo," alisema Kamanda Mayala.

Aliongeza kuwa, katika tukio hilo Bw. Mashaka Abdallah ambaye ni dereva, alijeruhiwa vibaya na kulazwa Hospitali ya Serikali wilayani Mbarali na hali yake inaendelea vizuri; watu wengine wawili walipatiwa matibabu na kuruhusiwa.

Alisema polisi waliokuwa doria eneo la Igawa, Mbeya na Njombe walifika eneo la tukio na magari mengi yakiwemo yanayosafirishwa kwenda nje, yakiwa yamesimamishwa.
 
"Watu hao walipoona gari la polisi walikimbilia vichakani na magari hayo yaliondoka chini ya ulinzi wa polisi kuendelea na safari, watu 10 tunawashikilia kwa mahojiano," alisema.

Makongoro Nyerere: Msiponiachia Najiua.

makongoron

Makongoro Nyerere

MSHITAKIWA Makongoro Nyerere anayekabiliwa na kesi ya mauaji ameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imuachie huru akaishi na watoto wake au ajiue.
Makongoro alidai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Hellen Liwa, baada ya Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Inspekta Jackson Chidunda kudai upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
Makongoro, ambaye ameshitakiwa pamoja na mfanyabiashara maarufu Abubakar Marijan (50), ‘Papaa Msoffe’ aliomba mahakama imuachie huru kwa kuwa hana kesi, alikuwa anafanya kazi halali lakini ameambiwa ameua, kisa Sh milioni nane.

Makongoro Afunguka

“Tarehe nyingine kesi itakapotajwa naomba niachiwe nikakae na watoto wangu niende nikakae polisi, huko watajua pa kunipeleka kama kujiua nijiue,” aliomba Makongoro.
Hakimu Liwa aliahirisha kesi hiyo hadi Machi 11, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena. Aliutaka upande wa Jamhuri kuharakisha upelelezi. Jana Papaa Msoffe hakufika mahakamani hapo kwa madai kuwa anaumwa.
Makongoro Nyerere
Washitakiwa wanadaiwa Oktoba 11, mwaka 2011 katika eneo la Magomeni Mapipa, jijini Dar es Salaam kwa makusudi walimuua Onesphory Kituli.
Hawakujibu mashitaka kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo isipokuwa Mahakama Kuu na wataendelea kusota rumande kwa kuwa mashitaka yao hayana dhamana.

Wananchi wataka Posho ya wabunge wa Bunge la Katiba ipunguzwe kutoka 300,000 hadi 170,000


Bunge la Katiba
WAKAZI wa wilaya za Tarime na Rorya mkoani Mara, wameshauri kupunguzwa kwa posho za wajumbe wa Bunge maalumu la Katiba kutoka Sh 300,000 hadi Sh 170,000 ambazo walisema ni za kawaida kwa vikao vya Bunge.
Wamewaomba pia wajumbe hao ambao wamekwenda kuwawakilisha wenzao kuweka maslahi ya Taifa mbele na kuacha tamaa za kujipatia fedha nyingi ambazo ni kodi za wananchi.
Waliotoa ushauri huo ni Sigirya Mwita ambaye ni Mwenyekiti wa CCM wa Kata ya Pemba, Peter Mwera ambaye ni Diwani wa CCM wa Kata ya Mriba na Nyangoko Paulo ambaye ni Mwenyekiti wa Kijiji Sirari kupitia Chama cha Chadema.
Wengine ni wananchi wa kawaida Otieno Igogo, Matiko Majani, Elizabeth Mseti, Ores Lameck, Kansela Sereria, Maria Bhoke na Gimase Marwa.
Viongozi na wananchi hao walisema hawakubaliani na maombi ya wabunge hao ya kuomba serikali kuwaongezea posho na badala yake wapunguziwe kutoka Sh 300,000 za sasa hadi Sh 170, 000 ambazo ndizo zinazokubalika kisheria kwa vikao.
“Katiba hii wanayoijadili ni ya Watanzania wote hata wao wamo na familia zao. Hawakupendekezwa kwenda kujitafutia mitaji na kutaka kuhujumu uchumi wa nchi. Kuna baadhi yao humo hawapati au kuzalisha hata Sh 100,000 kwa siku kwao.
“Kisingizio kuwa ni wajumbe wa Bunge maalumu la Katiba hakina mashiko.Tunaomba Serikali kutowaongeza posho hizo badala yake zipunguzwe kwani fedha hizo ni za wananchi ambazo zingine hupelekwa katika kutekeleza miradi ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa madarasa, nyumba za walimu, barabara, kuchimba visima vya maji na kuwasomesha wanafunzi waliokwama kuendelea na masomo,” walisema kwa nyakati tofauti.

DAKTARI FEKI AKAMATWA TENA MUHIMBILI AKITAPELI WAGONJWA


Hospitali ya taifa ya Muhimbili imemkamata mtu mmoja anae sadikiwa kuwa daktari feki ambaye kwa kipindi kirefu amekuwa akitapeli wagonjwa wanaoenda kutibiwa katika hospitali hiyo ya taifa kwa namna mbalimbali

Daktari huyo aliyejulikana kwa jina la Kitano Mustafa Kitani mwenye umri miaka 51 anadaiwa kuwa alikuwa anajitambulisha kama daktari upande wa akina mama katika hospitali ya Muhimbili.

Hospitali ya taifa ya Muhimbili mbali na utaratibu wa kutumia vitambulisho kwa wafanyakazi ili kuondoa tatizo kama hili, bado tatizo hili limeendelea kujitokeza.

Hospitali ya Muhimbili inawataka wafanyakazi wake wanaoshirikiana na madaktari vishoka kuacha tabia hiyo yenye athari kwa wagonjwa na taifa.

Chama cha Madaktari nchini kimewataka wananchi kuwa  macho na madaktari wanaojitokeza kutaka kusaidia wagonjwa.

Wakati daktari huyo akidai yeye ni daktari kitaaluma, Afisa Usalama hakubaliani nae kutokana na taarifa za kiuchunguzi kuthibitisha kuwa ni feki.

Hili ni tukio la tatu kutokea katika hospitali ya Muhimbili.

Monday, February 24, 2014

Museveni Ambwatukia Obama…Amtaka Aache Kuingilia Siasa za Uganda..!

Museveni

Raisi Yoweri Museveni.

Rais Yoweri Museveni wa Uganda ametoa matamshi makali dhidi ya Rais Barack Obama wa Marekani akimtaka akome kungilia masuala ya ndani ya Uganda.
Matamshi hayo makali yamekuja baada ya Rais wa Marekani kutishia kuwa uhusiano wa nchi yake na Uganda utaharibika iwapo Rais Museveni atasaini na kuufanya kuwa sheria muswada wa kupinga vitendo vichafu vya kujamiiana watu wa jinsia moja.

Agusia Kushirikiana na Russia.

Rais Museveni amesema, atashirikiana na Russia iwapo Marekani itaendelea kuingilia masuala ya ndani ya Uganda na kuongeza kama ninavyomnukuu:
“Russia imekuwa ikifanya shughuli zake barani Afrika tangu mwaka 1917 yaani kwa zaidi ya miaka 100. Ninataka kushirikiana na Russia kwa sababu hawachanganyi siasa zao na siasa za nchi nyingine.” Mwisho wa kunukuu.
Museveni
Rais Yoweri Museveni
Ameongeza kuwa: “Ukiona mtu anaingia ndani ya nyumba ya mtu mwingine basi jua kuna tatizo. Hapa ni nyumbani petu. Huwezi kumuona mtu mwenye upaa kama mimi hivi ndani ya nyumba yake na kuanza kumpangia afanye unavyotaka wewe. Rudi kwenu!” Alisema Rais Museveni

Sunday, February 23, 2014

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE SHULE ZENYE MAJINA YA VIONGOZI AIBU, YENYE JINA LA MKAPA YAFANYA VIZURI

Rais Benjamini Willium Mkapa, ambaye ndiye pekee jina lake linatumika vyema kwa shule iliyobeba jina lake kufanya vyema.
 
Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne 2013 yalitangazwa juzi na Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) Jijini Dar es Salaam. Blogu hii leo imepitia na kuangalia baadhi tu ya Shule za Sekondari ambazo zinamajina ya Viongozi wa Kuu wa Serikali, ama Wastaafu au waliopo madarakani. Lakini Matokeo hayo hayaendani kabisa na Majina hayo kutokana na vile zilivyofanya vibaya jambo ambalo ni aibu. 

Je ipo haja ya Viongozi hao kuhakikisha wanazisimamia shule hizo kwa ukaribu zaidi na kuhakikisha zinafanya vizuri ili kuepusha aibu iliyopo? au ziendelee hivi na viongozi hao wakijivunia kuwa jamii imewapa heshima ya Jina lake kutumika katika shule tu. Angalia baadhi ya matokeo ya shule hizo ambazo ni Benjamini Mkapa tu inaonesha walau kufanya vyema. 

S0960 BENJAMIN WILLIAM MKAPA HIGH SCHOOL
DIV-I = 45 DIV-II = 52 DIV-III = 56 DIV-IV = 92 DIV-0 = 65

S1930 J. M. KIKWETE SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 2 DIV-II = 2 DIV-III = 13 DIV-IV = 54 DIV-0 = 43

S0817 PAUL BOMANI SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 0 DIV-II = 1 DIV-III = 4 DIV-IV = 36 DIV-0 = 32

S0861 NELSON-MANDELA SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 0 DIV-II = 0 DIV-III = 2 DIV-IV = 30 DIV-0 = 70


S0922 MWINYI SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 0 DIV-II = 4 DIV-III = 11 DIV-IV = 21 DIV-0 = 41

S0985 MZINDAKAYA SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 0 DIV-II = 1 DIV-III = 3 DIV-IV = 31 DIV-0 = 26

S1033 AMANI ABEID KARUME SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 0 DIV-II = 0 DIV-III = 2 DIV-IV = 26 DIV-0 = 53

S0614 NYERERE SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 1 DIV-II = 1 DIV-III = 9 DIV-IV = 54 DIV-0 = 64

S0716 MALECELA SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 1 DIV-II = 6 DIV-III = 20 DIV-IV = 73 DIV-0 = 19

S0740 ALI HASSAN MWINYI ISL. SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 0 DIV-II = 9 DIV-III = 35 DIV-IV = 101 DIV-0 = 103

S1038 J.K. NYERERE SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 13 DIV-II = 35 DIV-III = 40 DIV-IV = 110 DIV-0 = 53

S1344 MWALIMU J K NYERERE SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 3 DIV-II = 10 DIV-III = 19 DIV-IV = 47 DIV-0 = 54

S1728 RASHIDI MFAUME KAWAWA SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 0 DIV-II = 1 DIV-III = 2 DIV-IV = 14 DIV-0 = 16

S1796 DR. DIDAS MASABURI SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 1 DIV-II = 5 DIV-III = 22 DIV-IV = 26 DIV-0 = 2

S1806 YUSUF MAKAMBA SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 0 DIV-II = 9 DIV-III = 33 DIV-IV = 92 DIV-0 = 112

S1803 LOWASSA SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 2 DIV-II = 9 DIV-III = 25 DIV-IV = 72 DIV-0 = 71

S1812 ISDORE SHIRIMA SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 0 DIV-II = 0 DIV-III = 0 DIV-IV = 7 DIV-0 = 20

S3561 SALMA KIKWETE SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 6 DIV-II = 19 DIV-III = 24 DIV-IV = 91 DIV-0 = 77

S3725 FELIX MREMA SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 2 DIV-II = 9 DIV-III = 36 DIV-IV = 93 DIV-0 = 77

S4029 WILLIAM LUKUVI SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 0 DIV-II = 3 DIV-III = 3 DIV-IV = 21 DIV-0 = 8

S5068 JOEL BENDERA SECONDARY SCHOOL
DIV-I = 0 DIV-II = 0 DIV-III = 5 DIV-IV = 6 DIV-0 = 28

TUKIO LA AINA YAKE:- MKE WA MWANAUME APATA MIMBA NJE YA NDOA NA KUTUPA MTOTO MCHANGA CHOONI CHEKI LAIVU HAPAAAAAAA!!!


Rukia Fungameza[20]mkazi wa mtaa wa Ilembo Kata ya Iwambi Mbeya, Anaetuhumiwa kutupa mtoto chooni


Hii ndilo shimo la choo alimotumbukizwa mtoto huyo

MAGAZETI YA LEO JUMATATU 24-02-2014



.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.


.

Diego Maradona Kurudi Uwanjani Tena Na Timu Atakayochezea iko Hapa.

Nyota wa kimataifa kwenye soka ambaye ni mchezaji mwenye umri wa miaka 53 kutoka  Argentina Diego Maradona amekuwa katika mazungumzo na klabu
ya Deportivo Riestra, ambayo inashiriki ligi ya chini kabisa  kwa lengo la kujiunga nao kama mchezaji mpaka kumalizika kwa msimu.
Nchini kwake ni maarufu kwa jina ‘God’  Maradona amekuwa akipambana na uzito katika siku za hivi karibuni kwa lengo kujiweka sawa na fiti  kabla ya kuanza mchezo wake wa kwanza March 23.
Mmoja wa wachezaji wa Deportivo Kiungo Victor More, amesema yuko tayari kuvua jezi yake nambari 10 anayovaa sasa na kumkabidhi Maradona atakapo saini kuichezea klabu hiyo na pengine mkongwe huyo anayetumia mguu wa kushoto akarejea kuitendea haki jezi hiyo aliyokuwa akiivaa enzi zake.

BAADA YA KULALAMIKA, SASA POSHO YA WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA KUWA SH. 500,000/=



Posho Bunge Maalumu la Katiba kuwa 500,000 kwa siku.

Habari zilizoandikwa na gazeti la Mtanzania la jana kwamba Kamati ya kufuatilia posho za wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba imependekeza kwa Rais posho ya tshs 500,000 kwa siku imethibitishwa ni kweli.


Natoa wito kwa Wananchi wote kushinikiza kwa Rais pendekezo hili asilikubali. Naunga mkono wazo la mjumbe wa Bunge Maalum ndg Julius S. Mtatiro la kuorodhesha majina ya wote wanaopinga nyongeza ya posho. Nitaweka sahihi kwenye petition yake hiyo mapema kesho asubuhi.


Wagombea uenyekiti nao wanaahidi kupandisha posho. Nawaonya wasithubutu kutoa ahadi hiyo kwani sio mamlaka yao. Mgombea mwenye sera ya posho hatapata kura yangu na nitashawishi wajumbe wengine wasimpe kura.

Friday, February 21, 2014

ANGALIA MATOKEO YOTE YA KIDATO CHA NNE 2013-TANZANIA HAPA


f



 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MATOKEO YOTE YA KIDATO CHA NNE 2013-TANZANIA

 

http://41.188.155.122/CSEE2013/olevel.htm

Thursday, February 20, 2014

WATAALAMU CHUO KIKUU WATOA RIPOTI YA UZIMAJI WA MITAMBO YA ANALOGIA AWAMU YA KWANZA

wasomi
1.0  UTANGULIZI
Mamlaka ya Mawasiliano imepokea matokeo ya tathmini ya zoezi la uhamaji toka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda kidijiti. Zoezi hili lilifanyika kwenye miji saba kama ilivyotajwa kwenye taarifa iliyotolewa na wataalamu wa Chuo kikuu cha Dar e salaam waliofanya tathmini ya Uzimaji wa Mitambo ya Analojia katika Awamu ya Kwanza.Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilifanya kamisheni kwa Chuo Kikuu cha Dar es salaam kufanya tathmini ya uzimaji wa Mitambo ya Analojia katika Awamu ya Kwanza, ikitambua kuwa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kuna wataalamu wenye uzoefu mkubwa wa kufanya tathmini za aina mbalimbali, na kwamba uzoefu huo utasaidia sana kuhakikisha kuwa tunapata taarifa ya uhakika itakayotuwezesha kuboresha zoezi hili kwenye awamu inayofuata.Nachukua nafasi hii kuwapongeza wataalamu waliohusika katika tathmini hii kwa weledi wao kwenye kazi hii muhimu kwa taifa letu kulingana na matokeo yaliyowasilishwa kitaalamu mbele yenu waandishi wa habari leo hii.Tanzania ni nchi ya kwanza kuzima mtambo ya analojia Barani Afrika. Uamuzi wa kufanya hivyo, na matokeo yake, umeiletea sifa kubwa nchi yetu kwa jinsi ambavyo Tanzania ilijipanga na kutekeleza maazimio yaliyofikiwa kimataifa kwa wakati na weledi mkubwa. Hii imeonyesha wazi jinsi Serikali ilivyoweza kushirikiana na taasissi zake pamoja na wadau wote katika kutimiza azma hii iliyoafikiwa kimataifa tangu 2006.Zoezi la uzimaji mitambo kwa awamu ya kwanza iliyoanza taree 31 disemba 2013 halikuwa rahisi kama wengi wetu tunavyoweza kufikiria, kwani liligusa nyanja nyingi zikiwemo za kijamii, kibiashara, kiufundi na Kisiasa. Mamlaka kama mdhibiti wa sekta ya Mawasiliano, ilibidi kuzingatia matakwa ya nyanja zote na wadau mbalimbali bila kuathiri utoaji wa habari nchini. Inakadiriwa kuwa mpaka kumaliza zoezi hili, mitambo ya kurushia matangazo kwa mfumo wa analojia isiyopungua 60 itakuwa imezimwa. Hali hii imefanya Tanzania kuwa nchi ya pekee na kuifanya nchi yetu kuwa kituo cha mafunzo kwa nchi nyingi ambazo sasa zimekuwa zikifika kujifunza hapa nchini.
Uamuzi wa kufanya mkutano wa nchi za SADC na ule wa nchii za Jumuiya ya Madola kuhusu Mfumo mpya wa utangazaji wa kidijiti kwa sekta ya utangazaji hapa nchini hivi karibuni, ni matokeo ya mafanikio makubwa tuliyo yapata kwenye zoezi hili lililoendeshwa kitaalamu na Serekali yetu kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
2.0  UPELEKAJI WA MKONGO WA TAIFA KWENYE VITUO VYA KURUSHIA
MATANGAZO
Mamlaka ya Mawasiliano kwa kushirikiana na Wizara na Kampuni ya Simu ya TTCL tuko kwenye mchakato wa kuhakikisha kuwa vituo vyote vya kurushia matangazo vinafikiwa na mkongo wa Taifa (Optic fiber cable).
Madhumuni ya jitihada hizi, ni kuona kuwa mbali na huduma ya msingi ya kurusha matangazo ya televisheni, vituo vya utangazaji vinatoa huduma za ziada zipatikanazo kwenye mfumo wa kidijiti. Kwa lugha ya kitaalam ni “interactive services”. Napenda kuchukua nafasi hii kuvitaka vituo vya utangazaji vyote nchini kuwa wabunifu na kutumia fursa zilizopo kwenye teknolojia hii ya kidijiti ili wananchi waweze kuona tofauti kubwa kati ya mfumo wa zamani wa analojia na huu mpya wa kidijiti.
3.0   UZIMAJI MITAMBO YA ANALOJIA AWAMU YA PILI
Baada ya kupokea matokeo ya tathmini Awamu ya Kwanza, Mamlaka ya Mawasiliano inajipanga kuzima mitambo kwa awamu ya pili na ya mwisho. Katika awamu hii, inategemewa miji 12 itahusika na uzimaji wa mitambo ya analoja. Lakini kama maafikiano yalivyofanyika awali, uzimaji utafanyika tu pale ambapo huduma za utangazaji wa kidijiti umefika.  Vigezo vyote vitano tulivyokubaliana na wadau vitahakikishwa kuwa vinatimizwa kabla ya kuzima mitambo hiyo.
Ni matarajio ya Mamlaka kuwa wasimikaji wa mitambo ya kidijiti (Multiplex Operators) wataendelea kwa kasi ufungaji wa mitambo hiyo hasa kwenye maeneo ambayo mfumo wa analojia unatumika. Mpaka sasa miji mingine 7 inapata huduma ya matangazo ya kidijiti nayo ni Morogoro, Singida, Tabora, Musoma, Kigoma, Bukoba na Kahama. Mchakato wa kufunga mitambo ya kidijiti kwenye miji iliyobaki inaendelea vizuri. Tunatarajia kuwa vituo vya utangazaji vitatoa ushirikiano mkubwa kama ule tulioupata kwenye awamu ya kwanza.
 Mamlaka imeyachukua mapendekezo yote yaliyotolewa kwenye ripoti hii na tunaahidi kuwa tutayafanyia kazi. Yale yaliyo nje ya uwezo wetu tutayafikisha mahali panapohusika kwa utekelezaji zaidi.
Mwisho, napenda kuwafahamisha kuwa Mamlaka imependekeza rasimu ya ratiba ya uzimaji mitambo awamu ya pili na ya mwisho itakayotangazwa na Waziri mwenye dhamana ya sekta ya Mawasiliano hivi karibuni.
Katika mapendekezo ya Mamlaka, tunakusudia kuanza awamu ya pili katika miji ya Singida na Tabora mnamo mwishoni wa mwezi Machi 2014. Miji mingine katika awamu ya pili itakuwa Musoma, Bukoba, Morogoro, Kahama, Iringa, Songea na Lindi. Awamu ya pili inategemewa kukamilika mwishoni mwa mwezi Oktoba 2014.
Nia ya Mamlaka ni kuona zoezi hili la uhamaji kutoka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda mfumo wa kidijiti linakamilka katika nchi yetu kabla ya kufikia ukomo wa matangazo ya analojia kama ilivyoelekezwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia Mawasiliano Duniani (ITU) siku ya tarehe 17 Juni 2015.
Imetolewa na:
MKURUGENZI MKUU
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
19 February 2014

Dijitali yatawala Bungeni kudhibiti ulopokaji Bunge la Katiba..!

bunge1
BUNGE Maalumu la Katiba, limeanza chini ya mfumo wa kidijitali ambao pamoja na masuala mengine, vipaza sauti vyote viko chini ya udhibiti wa Mwenyekiti hali ambayo haitaruhusu mbunge kuvitumia bila ridhaa ya kiti.
Hayo yalifahamika jana bungeni mjini hapa, wakati Sekretarieti ikitoa maelekezo kwa wajumbe kuhusu ukaaji na jiografia ya ukumbi.
Aidha wajumbe wamehakikishiwa kuwepo usalama wa kutosha huku wakiambiwa wakubaliane na upekuzi wa hali ya juu unaofanyika kutokana na mazingira ya sasa ambayo suala la usalama ni tata.
Chini ya usimamizi wa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah na Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Yahya Khamis Hamad, ilielezwa, Mwenyekiti wa Bunge Maalumu sasa anao uwezo wa kuzima kipazasauti za mjumbe akiwa mezani kwake.
“Sauti ya kaa chini ikisikika, ukitaka kuendelea kuzungumza, sauti haitasikika,” alisema Kaimu Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari (IT), Didas Wambura.
Kutokana na mfumo huo, kipaza sauti cha kwanza kikishawashwa, kinaonesha rangi nyekundu.
Wengine wakiwasha, wanaoneshwa rangi ya kijani kuashiria kwamba wasubiri. Viashiria hivyo vinakuwa kwenye kiti ambaye anavitumia kuruhusu wazungumzaji.
Mfumo utaweza? Hata hivyo muda mfupi baada ya wataalamu kuwasilisha maelekezo, walipopewa muda wa kuuliza maswali au kupata ufafanuzi, walijitokeza wajumbe wengi waliotaka kuzungumza ambao baadhi, baada ya kudhibitiwa na mfumo, walipaza sauti bila kutumia vipaza sauti wakitaka wapewe nafasi.
Wakati huo huo Wambura alisema kila mjumbe ana kadi inayomwezesha siyo tu kufungulia mlango, bali kutumia katika kuzungumza kupitia vipaza sauti hivyo na pia inamwezesha kupiga kura.
Kaimu Mkuu wa Usalama wa Bunge, Peter Magati alisema wameongeza vituo vya upekuzi na akaomba wajumbe wakubaliane na hali hiyo.
“Mazingira ya sasa hivi ya hali tata ya usalama ndiyo sababu ya upekuzi wa namna hii,” alisema.
Aliendelea kusema, “tumejiandaa kuhakikisha mnakaa kwa amani na utulivu ndani na nje ya Bunge.” Kuhusu wageni, alisema watakuja kwa taarifa na akataka wajumbe kuhakikisha wageni wao wanakuwa katika mavazi ya staha yasiyo na walakini. Masuala mengine waliyohakikishiwa wajumbe, ni umeme kutokatika.
Sanjari na hilo, Mkuu wa Wakala wa Serikali Mtandao, Dk Jabir Bakar alisema pia ipo Wavuti ya Bunge Maalumu itakayokuwa ikirusha shughuli zote za Bunge moja kwa moja sanjari na Televisheni ya Taifa (TBC).
Huduma za matibabu zinapatikana katika hospitali iliyoko bungeni na ikitokea matibabu yakashindikana, mjumbe anaruhusiwa kwenda hospitali nyingine ya Serikali au binafsi kwa ushauri wa daktari na gharama za matibabu zitarudishwa.
Aidha wajumbe wamepewa orodha ya hoteli huku wakiaswa kutokwenda maeneo yanayohatarisha maisha yao.
Posho Taarifa ya Mhasibu Mkuu wa Bunge ilieleza kwamba licha ya wajumbe kulipwa posho ya kujikimu kila siku huku posho maalumu ikilipwa kwa wiki, vile vile wenye wasaidizi watalipwa posho ya kujikimu.
Malipo mengine wanayopewa wajumbe ni gharama za usafiri ambazo zitarejeshwa baada ya mhusika kuwasilisha tiketi ya usafiri aliotumia. Pia upo utaratibu wa kurudisha mafuta kwa waliotumia usafiri binafsi.
Wajumbe wenye watoto wachanga wameambiwa wawasiliane na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu kwa ajili ya kupewa utaratibu juu ya eneo la kutolea huduma.
Ukaaji ndani ya ukumbi huo wenye viti 676, umezingatia majina, wenye mahitaji maalumu hususani wenye ulemavu na pia wenye mahitaji maalumu ya kiusalama kama vile Waziri Mkuu.
Wajumbe Baada ya maelekezo kutolewa ukumbini, baadhi ya wajumbe walilalamikia masuala mbalimbali, wakiwemo wenye ulemavu waliotaka mazingira rafiki kwao ikiwemo kuwepo wakalimani kwenye televisheni.
Vile vile suala la usawa wa jinsia katika uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu wake, lilijitokeza kutoka miongoni mwa wajumbe. Mjumbe wa kwanza kusimama alikuwa Tundu Lissu, ambaye alitaka ufafanuzi kutokana na kile alichosema baadhi ya nyaraka muhimu hazimo kwenye makabrasha.
Mwingine, Mussa Ali Kombo, alilalamikia posho akisema wapo waliofika Februari 16 mwaka huu lakini hawakujisajili jambo ambalo limewanyima posho ya kujikimu. Alitaka wafikiriwe kupatiwa posho hiyo.
Ernest Kimaya alitaka kufahamu iwapo wenye ulemavu watapatiwa maandishi makubwa. Kwa upande wake, Amon Mpanju alihoji kama kutakuwepo wakalimani wa lugha za alama ili watu walio kundi hilo wafuatilie yanayojadiliwa kwenye Bunge.
Naye Julius Mtatiro alihoji kuhusu stahiki za wajumbe akitaka posho maalumu wanayopewa, viwango vitajwe waelewe. Kwa upande wake, Kangi Lugora alitaka wagawiwe mapema rasimu ya Kanuni za Bunge hilo.
“Iko tabia ya kuuziwa mbuzi kwenye gunia…tugawiwe haraka. Lazima tuwe na muda wa kutosha. Mpaka kieleweke mimi sitoki bila kuwa na kanuni,” alisema.
Hata hivyo Katibu wa Bunge, Dk Kashililah alisema suala la kanuni inabidi kusubiri apatikane Mwenyekiti wa Muda ambaye ndiye mwenye jukumu la kuandaa kanuni. Akizungumzia usawa wa kijinsia katika kupata Mwenyekiti na Makamu wake, Kashililah alisema uchaguzi huo ni suala la kisheria.
“Mnatubebesha mzigo tu, naliacha kwa mtaalamu,” aliwaambia wajumbe. Kuhusu maandishi makubwa na wakalimani kwa wenye ulemavu, Katibu wa Bunge alisema huduma hizo zitapatikana mkutano utakapoanza.
Aidha kuhusu hoja ya Lissu, Kashililah alikubaliana naye na akasema nyaraka zinaendelea kuchapishwa na kabla ya kuanza kupitia rasimu ya katiba, zitakuwa zimepatikana. Akijibu aliyelalamikia posho, Kashililah alisema ambao hawakulipwa posho ya kujikimu lakini walifika Dodoma Februari 16 wawasilishe uthibitisho.
Source: Habarileo

Wakenya Walalamikia Katiba Mpya Kuwalazimisha kulipa Ushuru wa Kuaga Maiti na Kuchinja Mifugo yao.


funeral
Kenya ilizindua Katiba mpya Agosti 27 mwaka 2010 kwenye sherehe iliyojaa mbwembwe katika bustani ya Uhuru,hatimaye katiba hiyo imeanza kuwapa machungu ya kulazimika kulipa ushuru wa kuaga maiti pamoja na kulipa ushuru wakuchinja mifugo yao.
Inatafsiriwa kuwa, magavana wametumia mamlaka yao kunyanyasa wananchi katika kaunti. Katika Kaunti ya Kiambu, inayoongozwa na Gavana William Kabogo, kuna ushuru mpya unaotozwa kwa familia iliyopoteza mpendwa ama wapendwa wao. Hakuna anayekubaliwa kumzika mfu wao bila kulipa ushuru huo. Pia, huwezi kuchinja mfugo wako nyumbani bila kulipa ushuru!
Katika Kaunti ya Kakamega, Gavana amebuni ushuru wa kuku ambapo kila mfugaji atalipa Sh20 kwa kila kuku anayemfuga.
Pia, watu wanapoomboleza, lazima walipe ushuru wa kuomboleza haswa wanapotazama mwili wa marehemu.
Ukiutazama zaidi ya mara mbili, utalipa ushuru zaidi ya mara moja!
Watu hawajui la kufanya na wana majuto makuu kwa kukaribisha Katiba mpya 2010. Walipokuwa wanaipitisha walikuwa na matumaini kwamba ingebadilisha maisha yao kwa kuleta utawala na huduma za Serikali Kuu karibu yao.
Wakati huo wa mchakato wa Katiba mpya, Makamu wa Rais William Ruto alikuwa katika upande uliokuwa ukipinga Katiba hiyo.
Source:Mwananchi

Wabunge waikataa posho ya sh 300,000 kwa siku….Wanadai eti ni ndogo sana na haziendani na hadhi zao

bunge1
WAKATI mjadala wa kihistoria wa kuunda Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ukiwa katika hatua ya kupata kanuni za Bunge Maalumu la Katiba, baadhi ya wajumbe wameamua kuelekeza nguvu kudai posho nono. 

Wajumbe hao wanapinga posho ya sasa ya Sh 300,000 kwa siku, ambayo kwa wananchi wa kawaida inaonekana ni kubwa, lakini vielelezo vyao ni taarifa, kwamba wajumbe ambao wanatoka Baraza la Wawakilishi, wanalipwa zaidi ya hapo.
 
Mbali na hoja hiyo ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, ambayo sasa wajumbe ambao ni wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, wanafikiria kumbana Spika Anne Makinda, ili nao waongezwe posho kama wenzao wa Zanzibar, hoja nyingine imetajwa kuwa ni hadhi ya wabunge kwamba haifanani na Sh 300,000.
 
Aliyeanzisha hoja hiyo jana ni Richard Ndassa, Mbunge wa Sumve, ambaye mbali na kutaka nyongeza ya posho, alipinga utaratibu wa kusaini asubuhi na jioni kwa ajili ya posho zinazotolewa ‘rejareja’, akipendekeza waaminiwe na walipwe fedha nyingi kwa mkupuo.
 
Mjumbe mwingine, Suleiman Nchambi, alimwunga mkono Ndassa, lakini akahoji iweje wajumbe wa Tume ya Kurekebisha Katiba walipwe posho kubwa nao walipwe kidogo.
 
Mezani kwa Serikali
Kutokana na hoja hizo, Mwenyekiti wa muda wa Bunge, Pandu Ameir Kificho, alisema suala hilo linachukuliwa kwa umuhimu na watazungumza na Serikali liamuliwe baadaye.
 
“Kuhusu masuala ya posho, kama nilivyosema tunalichukua ili tuangalie uwezekano wa kuzungumza na Serikali, hili tutaamua hapo baadaye,” alisema Kificho.
 
Tume Akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge, Ndassa alisema wajumbe wa Tume walikuwa wakilipwa Sh 500,000 kwa siku huku madereva wakilipwa Sh 220,000.
 
“Mimi ninayehangaika kuanzia asubuhi na mimi nalipwa Sh 220,000? Mimi mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba na dereva wa Tume ni sawa?” Alihoji Ndassa.
 
Katika Sh 300,000 kwa siku, Sh 80,000 ndiyo posho ya kujikimu ambayo wajumbe wa Bunge la Katiba watapewa kila siku, iwe amefanya kazi au la, na Sh 220,000 ni posho ya kazi, ambayo itatolewa kwa waliofanya kazi tu.
 
Hadhi ya Mbunge “Mimi kwenye hizi laki tatu (Sh 300,000) zangu zote, ni pamoja na dereva wangu, simu, chakula, mafuta, lakini pia unamtaka mbunge eti lazima asaini kwanza!” Alionesha mshangao.
 
Bila kupendekeza kiwango cha kulipwa, Ndassa alitoa mchanganuo wa matumizi ya mbunge, akisema hoteli ya hadhi yake ni Sh 70,000 kwa usiku mmoja.
 
Mbali na gharama hiyo ya malazi, alisema gharama za chakula, mafuta ya gari, dereva na msaada atakaotakiwa kutoa kwa watu mbalimbali Sh 80,000 haitoshi.
 
“Hoja yangu ya msingi, ni kwamba Serikali ijaribu kuangalia suala hili kwa upana, tukiliacha hivi hivi linaweza kuleta tatizo,” alisema Ndassa.
 
Kususa
Ndassa alisema wabunge wengine ni wafanyabiashara ambao hawawezi kukubali kukaa bungeni kwa muda wote wakilipwa posho ya Sh 300,000.
 
Alipohojiwa anatarajia mtazamo gani kutoka kwa wananchi wanaoishi kwa kipato cha chini ya dola moja kwa siku (Sh 1,600), huku yeye akikataa Sh 300,000 kwa siku, Ndassa alisema: “Ukiweka matarajio ya jamii itasemaje, huwezi kufanya kazi. Maswali kama hayo huwezi kuyakwepa, binadamu hamwezi kulingana nyote duniani, hata vidole viko tofauti.”
 
Nchambi alisema kwa upande wao, wabunge hawana tatizo isipokuwa anatetea wajumbe wengine ambao hawalipwi kiinua mgongo wala mshahara.
 
“Mbunge anatakiwa alale kwenye hoteli ya angalau Sh 70,000. Hata wananchi wanatakiwa waelewe kwamba wabunge wamekuja kufanyia kazi Katiba ambayo ndiyo msingi wao,” alisema Nchambi.
 
Ubaguzi
Suala lingine lililoibuliwa na Ndassa nje ya ukumbi, ni kuhusu tofauti ya kiasi cha posho kwa alichosema wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, wameongezwa Zanzibar wakati wengine wakipokea Sh 300,000.
 
Bila kutaja kiasi kilichoongezwa, Ndassa alisema:“Lakini wenzetu Wazanzibari wameongezwa na Baraza la Wawakilishi, wote ni wajumbe wa Bunge hilohilo… lazima kutakuwa na mgawanyiko. Na sisi tukisema hawa wabunge wamekwenda kwao wameongezwa na sisi tumwambie Makinda atuongeze, hawa makundi maalumu watakwenda kuongezwa wapi?
 
“Kwa kufanya hivyo umeshaweka mgawanyiko inatakiwa tuwe kitu kimoja, kama ni Sh 20 wote tupewe Sh 20, kama ni Sh 800 wote tuwe sawa,” alisema Ndassa.
 
Mwandishi wa habari hizi hakufanikiwa kumpata Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Yahya Khamis Hamad kufafanua hilo kutokana na kuwa kwenye kikao.
 
Lakini taarifa kutoka kwa baadhi ya watendaji wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), zilithibitisha kwamba wawakilishi waliomba waongezwe Sh 500,000 lakini hawakupewa zote; wamepewa chini ya hapo.
 
“Si kweli (hawapokei Sh 420,000) lakini waliomba Sh 500,000 ila hawakupewa hizo, wamepewa chini ya hapo,” alisema mtoa habari ambaye hakusema ni kiasi walichoongezwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.
Utaratibu
Kwa mujibu wa Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah, wabunge hao wameshapewa posho ya kujikimu ya Sh 80,000 kwa siku kuanzia Februari 16 hadi 28.
 
Aliongeza kuwa posho maalumu ya kazi ya Sh 220,000 kwa siku, ambayo hupigiwa hesabu kutokana na ushiriki wa mjumbe kusaini mahudhurio kila siku asubuhi na jioni, itakuwa ikiingizwa kwenye akaunti za wajumbe kila baada ya wiki moja ya kazi.