Sunday, February 23, 2014

Diego Maradona Kurudi Uwanjani Tena Na Timu Atakayochezea iko Hapa.

Nyota wa kimataifa kwenye soka ambaye ni mchezaji mwenye umri wa miaka 53 kutoka  Argentina Diego Maradona amekuwa katika mazungumzo na klabu
ya Deportivo Riestra, ambayo inashiriki ligi ya chini kabisa  kwa lengo la kujiunga nao kama mchezaji mpaka kumalizika kwa msimu.
Nchini kwake ni maarufu kwa jina ‘God’  Maradona amekuwa akipambana na uzito katika siku za hivi karibuni kwa lengo kujiweka sawa na fiti  kabla ya kuanza mchezo wake wa kwanza March 23.
Mmoja wa wachezaji wa Deportivo Kiungo Victor More, amesema yuko tayari kuvua jezi yake nambari 10 anayovaa sasa na kumkabidhi Maradona atakapo saini kuichezea klabu hiyo na pengine mkongwe huyo anayetumia mguu wa kushoto akarejea kuitendea haki jezi hiyo aliyokuwa akiivaa enzi zake.

No comments:

Post a Comment