Sunday, August 24, 2014

Taarifa ya kufungwa kwa kipande cha barabara ya Mandela-Ubungo

kielelezo

Mkandarasi Mkuu anayeshughulikia mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam, Strabag International ametangaza kufungwa kwa muda kipande cha barabara ya Mandela hadi makutano ya Ubungo Mataa.

Ofisa Uhusiano wa kampuni hiyo Bw. Yahya Mkumba amesema kipande cha barabara ya Mandela kuanzia makutano ya barabara ya Morogoro upande wa kushoto uelekeo wa Tabata kuanzia Ubungo Mataa hadi Darajani patafungwa kuanzia tarehe 25/08/2014 mpaka tarehe 30/08/2014 ili kupisha ujenzi.
Watumiaji wa barabara hiyo watalazimika kutumia upande mmoja wa barabara hiyo. Magari yatakayokuwa yanatokea Mwenge, Kimara na Shekilango yatalazimika kutumia barabara ya upande wa kulia ambayo pia itakuwa ikitumika na magari yanayotoka Tabata kuelekea Ubungo.

“Tunaomba radhi kwa usumbufu utakaotokea,” alisema Bw. Mkumba.

No comments:

Post a Comment