Wednesday, April 30, 2014

Lishe asili ni dawa ya wagonjwa wa moyo

140430034802_kula_vyakula_asili_inazidisha_miaka_ya_wagonjwa_wa_moyo_512x288_bbc_nocredit_c9f25.jpg
 Wanasayansi nchini Marekani wanasema watu waliowahi kupata maradhi ya moyo wanaweza kuishi maisha marefu iwapo watakula zaidi vyakula ambavyo havijapitia viwandani.
Watafiti walichunguza zaidi ya watu elfu nne waliowahi kupata mshituko wa moyo na kubaini kuwa wana uwezekano mkubwa wa kuishi miaka tisa zaidi kama watakula vyakula hivyo .
Vyakula ambayo havijapitia viwandani vina nyuzinyuzi ambazo tayari imethibitishwa kuwa husaidia katika kuwezesha binadamu kwenda haja bila matatizo.
Vyakula ambayo vina nyuzinyuzi hizo ni kama vile matunda, mboga na nafaka.
Hatahivyo wataalam wanasema watu katika mataifa mengi hawali vyakula hivyo kwa wingi.CHANZO BBC

No comments:

Post a Comment