Wednesday, April 30, 2014

DC NJOMBE AWATAKA WAZAZI KUWASILISHA CHAKULA KWA AJILI YA WANAFUNZI SHULENI


 
Mkuu wa wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba
 
Na Michael Ngilangwa
 
Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba amelejea tena kusisitiza kauli ya serikali ya kuwataka wazazi na walezi kuchangia chakula shuleni pamoja na kuwakamilishia mahitaji mbalimbali ya shule  ili kuwepo kwa mahudhurio mazuri ya wanafunzi na kuboresha kiwango cha taaluma.


Akizungumza na mtandao huu Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba ameziagiza kamati na bodi za shule mbalimbali zilizopo katika halmashauri  Ya Wilaya ya Njombe kuhakikisha zinasimamia ujenzi wa miundombinu  ya vyoo huku wazazi wakitakiwa kuwanunulia  mahitaji ya shule na kuwaweka watoto katika mazingira ya usafi.


Aidha bi.Dumba amesema kuwa katika ziara zake za kutembelea maeneo mbalimbali wilayani Njombe kukagua utekelezaji wa miradi  amebaini kuwepo kwa tatizo la baadhi ya shule kukosa huduma za chakula,wanafunzi kutokuwa na sale za shule pamoja na kukosekana kwa vyoo bora kwa maeneo yote ya shuleni na nyumbani.


Amesema kuwa kukosekana kwa huduma bora za vyoo zinaweza kusababisha mripuko wa magonjwa katika maeneo ya shule na nyumbani ambapo amewataka wataalamu wa afya wa kata na vijiji  kutembelea maeneo hayo ili kukagua na kuhimiza usafi wa mazingira  katika maeneo ya shule na makazi ya wananchi na kujikinga na mlipuko wa magonjwa hayo Huku kamati na bodi akizitaka kupeleka miundombinu ya maji kwa kushirikiana na wananchi ili vyoo  viweze kutumia maji.


Katika hatua nyingine Bi.Dumba amewataka wananchi kuepukana na unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na kwamba  hatua kali zinatakiwa kuchukuliwa kwa baadhi wanaoendekeza tabia hiyo ikiwa ni pamoja na kuwanyanyasa watoto huku akiwataka viongozi wa serikali za vijiji na kata kudhibiti tabia hiyo isiendelee kwani ni kitendo cha kumkandamiza mwanamke na mtoto.
 

No comments:

Post a Comment