Tuesday, March 4, 2014

AL AHLY WALIHAMA JIJI LA CAIRO, KILA KITU NI KIFICHO TU

Na Saleh Ally, Cairo
Mabingwa wa Afrika, Al Ahly ya hapa, wameamua kuondoka kwenye uwanja ambao wamekuwa wakifanyia mazoezi na kujichimbia kusikojulikana.
Al Ahly wameamua kufanya hivyo ili kufanya maandalizi yao kwa utulivu kabla ya kuivaa Yanga katika mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Jumapili.
Katika mechi ya kwanza jijini Dar es Salaam mabingwa hao wa Afrika walilala kwa bao 1-0 lililofungwa na nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' na kwa mara ya kwanza Yanga ikafuta uteja wa kufungwa kila inapokutana na Al Ahly.
Lakini mashabiki wao wengine wameeleza kuwa Ahly wameamua kujichimbia kutokana na vurugu zilizofanywa na mashabiki wake mara baada ya kupata taarifa kuwa wamefungwa bao 1-0 jijini Dar es Salaam.
"Wakati mwingine imekuwa kawaida Ahl kuondoka na kujificha sehemu kwa ajili ya maandalizi, lakini safari hii mambo yamekuwa tofauti kidogo, wanaonyesha wmepania kushinda mechi hii.
"Tokea wamerudi hawajaonekena klabu, huenda ni hofu ya mashabiki waliokuja kufanya vurugu hapa wakipinga wao kufungwa na timu kutoka Afrika Mashariki, lakini pia suala la umakini tu," alisema mmoja wa wafanyakazi kwenye uwanja huo kwa Kingereza cha tabu.
Championi lilifunga safari hadi kwenye uwanja huo jana mapema kutaka kushuhudia mazoezi yao, lakini likaambulia patupu na kuelezwa hivi: "Hutamuona mtu hadi siku ya mechi."

No comments:

Post a Comment